• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WAAGIZWA KUWEKA FEDHA ZA MAPATO BENKI KWA WAKATI –GEITA DC

Posted on: March 13th, 2024

Na: Hendrick Msangi

WATENDAJI wa Kata na Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wametakiwa kuweka fedha benki kwa wakati baada ya kukusanya tozo mbalimbali kama mapato ya Halmashauri kufuatia kuwepo kwa tabia ya watendaji hao kukaa na fedha za serikali kwa  muda mrefu bila kuziweka benki.

Maelekezo hayo yametolewa Machi 13, 2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo kilifanyika kikao elekezi kwa watendaji hao na timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Watendaji wa Kata na Vijiji kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa kwenye kikao ndani ya ukumbi wa Halmashauri ambapo kwa pamoja waliazimia kuweka fedha za mapato ya halmashauri ndani ya masaa 24 baada ya kukusanya katika vyanzo mbalimbali vya mapato kupitia mashine za kukusanyia ushuru (POS)

Wakizungumza kwa nyakati tofauti juu ya sababu zinazopelekea kutokuweka fedha za serikali kwa wakati na badala yake kukaa nazo muda mrefu hali ambayo inaipa Halmashauri sifa mbaya, watendaji hao wamesema changamoto kubwa ni kutoka kwa Mawakala kushindwa kufanya miamala hiyo kwa madai malipo ya kutumia control number hayawapi faida katika huduma wanazozitoa, baadhi ya maeneo kuwa na miundombinu isiyokuwa rafiki kuweka fedha ndani ya masaa 24 baada ya ukusanyaji.

Aidha changamoto nyingine zilizotajwa na watendaji hao ni ya kimfumo ambapo miamala inayojirudia kutoa stakabadhi kuchelewa kufutwa kwenye mfumo na wakati mwingine kutokusomeka kwenye mfumo kwa miamala inayolipwa kwa wakati huku changamoto nyingine ambayo ilibaina kwenye kikao elekezi hicho ni baadhi ya watendaji hao kuingia mikataba na vijana ambao huwasaidia katika zoezi zima la ukusanyaji wa mapato jambo ambalo limekuwa likiwaletea usumbufu pale ambapo wanatakiwa kuweka fedha benki na vijana hao kuchelewa kufanya kwa wakati.

Kikao hicho kilifikia maazimio ya pamoja kwamba fedha ya serikali inapaswa kuwekwa benki ndani ya masaa 24 baada ya makusanyo ya tozo mbalimbali katika vyanzo vya mapato vilivyopo kwenye mashine za kukusanyia mapato (POS). “Tumeazimia fedha zipelekwe benki ndani ya masaa 24 na iwapo muda huo hautazingatiwa sheria itachukua mkondo wake kwa kuwawajibisha watendaji wote watakaoshindwa kufanya hivyo na iwapo atakuwepo ambaye ana changamoto ya kushindwa kufanya hivyo awasiliane na Mwasibu wa Mapato kwa wakati” Alisema Bi Sarah Yohana akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji katika kikao hicho.

Pamoja na swala la kuweka fedha benki kwa wakati, watendaji hao waliaswa kuwa waadilifu katika maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kukata ushuru unaostahili kulingana na chanzo husika ambapo kwa wafanyabiashara wanaobeba bidhaa za mazao ya kilimo liliwekwa azimio la kukemea ubebaji wa rumbesa na iwapo mfanyabiashara atakutwa amebeba mzigo kwa kiwango cha rumbesa basi atozwe faini ili kukemea hali hiyo.

Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakifuatilia kikao elekezi kwa watendaji wa kata na vijiji ambapo maelekezo mbalimbali yalitolewa kwa watendaji hao ili kuendelea kuleta sifa njema kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Watendaji hao waliomba uongozi wa Halmashauri uangalie kata ambazo huduma za kifedha sio rafiki kuongezewa muda wa kupeleka fedha benki. “Hatupendi kukaa na fedha za serikali muda mrefu ila wakati mwingine changamoto ya uapatikanaji wa urahisi wa kuweka fedha inayokusanywa husababisha kuchelewesha kuweka fedha” alisema Martine Matiba mtendaji wa kata ya Ludete.

Aidha waliomba kupewa ushirikiano na watumishi wa Halmashauri pale wanapokamata magari ambayo yamebeba mazao bila kulipa ushuru stahiki. “Tunaomba tuaminike baada ya kupewa posi na sio kupewa maelekezo na baadhi ya wakuu wa idara kwa kuwakataza watendaji kukamata magari ya wanasiasa jambo ambalo ni changomoto na linawavunja moyo ikiwa ni pamoja na asilimia 10 itoke kwa wakati ili kusaidia watendaji kutekeleza majukumu yao kwa wakati” alisema Alfred Conrad mtendaji wa kata ya Izumacheri.

Timu ya Kikosi Kazi (Task Force) Ikiwa katika utekelezaji wa ukusanyaji wa mapato ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Wafanyabiashara wamekuwa wakitumia usafiri wa bodaboda na maguta kusafirisha mazao  kukwepa ushuru.

Kuhusu Kikosi Kazi (Task Force) kilichoundwa na timu ya menejimenti kwa ajili ya zoezi la ukusanyaji wa mapato, watendaji hao waliomba kuwepo kwa mahusiano mazuri kati yao na kikosi kazi ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa pindi Kikosi kazi kinapotembelea kwenye kata kwa ajili ya ukusanyaji wa mapato ambapo uongozi wa kata utasaidia upatikanaji wa mgambo pale inapohitajika kufanya hivyo katika zoezi zima la ukusunyaji wa mapato.

Naye mwenyekiti wa Watendaji wa Kata ndugu Lusekelo Mwaikenda kwa niaba ya watendaji aliushukuru uongozi wa Halmashauri kwa kufanya kikao na watendaji na kuomba kuendelea kuwepo kwa ushirikiano kati ya  watendaji na watumishi ili kuendelea kuinua mapato ya Halmashauri na kuahidi yote waliyo elekezwa kuyafanyia kazi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa