• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WAASWA KUZINGATIA ULAJI MZURI WA LISHE KUEPUKANA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA- DC KOMBA

Posted on: November 1st, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba, Oktoba 31,2024 amewataka wananchi Wilayani Geita kuzingatia Lishe bora katika maisha yao ya kila siku.

Wito huo umetolewa katika Kata ya Nzera yalipo Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo maadhimisho ya kilele cha siku ya Lishe yenye kauli mbiu “Mchongo ni Afya yako, Zingatia unachokula" yamefanyika.

Akizungumza na wananchi waliojotokeza katika maadhimisho hayo, Mhe Komba amewataka wazazi na wananchi kujenga tabia ya kutafuta na kutumia huduma za Lishe zinazopatikana kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

“Tujenge utamaduni wa kwenda kliniki pamoja akina baba na akina mama ili kupima afya kwa pamoja kwani itawapa faida za kupata elimu kusaidia makuzi ya watoto” amesisitiza Mhe Komba.

Mhe Hashim Komba amewataka akina baba kujenga desturi ya kuongozana na akina mama kwenda kliniki mara kwa mara.

Vilevile Mkuu wa Wilaya amezitaka familia kuzingatia mlo kamili  kwa kuzingatia wanachokula kwa kufuata mchanganyiko kutoka makundi 6 ya vyakula ili kuepuka magonjwa kama shinikizo la damu, kisukari, changamoto kwenye figo yanayoweza kusababishwa na mtindo wa ulaji mbovu wa lishe.

“Ukikosea kula vizuri ukala kwa kujaza tumbo yapo madhara utayapata ya magonjwa ambayo hukaribisha umasikini katika kuwahudumia wagonjwa hao , rai yangu tuitumie siku ya lishe kupata elimu kwa namna ambavyo tutakula katika maisha yetu. Ukiwa na Lishe bora umeimarisha afya za familia” amesema Mh Komba.

Aidha Mh Komba ameitaka Halmashauri kupitia idara ya afya, ustawi wa jamii na lishe kwa kushirikiana na idara mtambuka, wadau wa maendeleo na wananchi wote kuhakikisha elimu ya lishe inatolewa kuanzia ngazi ya kaya ili kuendelea kupambana na changamoto za udumavu na  utapiamlo.

Kwa upande wake Afisa Lishe (W) Bi Ummy Kileo amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kutoa elimu kwa jamii kuhusu afua za lishe.

Maadhimisho ya kilele cha lishe hufanyika kila ifikapo tarehe ya mwisho wa mwezi wa kumi kila mwaka ambapo yameenda sambamba na maadhimisho ya siku ya Afrika ya usalama wa chakula na lishe (Africa Day for Food and Nutrition Security-ADFNS).



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WATENDAJI WASIMAMIWE KUHAKIKISHA AFUA ZA LISHE ZINATEKELEZWA - MHE. KOMBA

    July 12, 2025
  • HALMASHAURI ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU KWENYE UKUSANYAJI WA MAPATO.

    July 12, 2025
  • VIKUNDI 111 VYANUFAIKA NA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA

    July 11, 2025
  • MHE. KOMBA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA OFISI YA KATA, BUGULULA.

    July 05, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa