• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

PLAN INTERNATIONAL WATOA VITABU 52,682 NA VIFAA MBALIMBALI VYA KITAALUMA ILI KUSAIDIA SEKTA YA ELIMU MKOANI GEITA

Posted on: August 31st, 2022

Na Michael Kashinde

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita katika maendeleo ya Sekta ya Elimu Shirika la Plan International limetoa vitabu 52,683, vifaa vya michezo pamoja na vifaa vya kujifunzia kwa watoto wenye ulemavu kupitia mradi wake wa miaka 5 wa kuwawezesha wasichana rika balehe kuendelea na masomo (Keeping Adolescent Girls in School - KAGIS) katika mkoa wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigela akizungumza katika hafla fupi ya kupokea vitabu hivyo Agosti 30, 2022 katika viwanja vya shule ya msingi Mkoani amelishukuru Shirika hilo kwa mchango wake katika maendeleo ya sekta ya Elimu na kwa kutekeleza malengo ya Milenia ya kumpatia elimu mtoto wa kike huku akisisitiza kuwa ukimwelimisha mwanamke umeielimisha jamii kwa kuwa mwanamke ni mchumi namba moja anapowezeshwa.

Mhe. Shigela ametoa wito wa kutumia vitabu hivyo kwa usahihi ili malengo yaliyotarajiwa yafikiwe huku akiishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia kwa kuongeza bajeti ya Elimu bila malipo sambamba kuleta kiasi cha Tshs. 470,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya kila jimbo kupitia mradi wa SEQUIP huku akiendelea kupiga marufuku kuzuia watoto kwenda shule kwa sababu ya kudaiwa michango mbalimbali.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo amelipongeza shirika hilo la Plan International kwa kuyajali makundi maalumu katika jamii wakiwemo watoto na watu wenye ulemavu sambamba na kuzisaidia sekta za Elimu, Afya na michezo huku akieleza kuwa Serikali inautambua mchango wao katika kujali na kuboresha mazingira na miundombinu ya watumishi  na wanafunzi mbalimbali.

Awali Bw. Nicodemas Gachu ambaye ni Mkurugenzi wa mradi wa KAGIS akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigella amesema kuwa mradi huo umelenga kushughulikia changamoto zinazozuia wasichana walio katika umri wa balehe kutambua haki yao ya Elimu salama, bora na inayozingatia jinsia.

Bw. Gachu ameendelea kwa kusema kuwa mradi unatekeleza ajenda ya kitaifa ya kuwekeza katika Afya na maendeleo ya vijana balehe kwa kulenga nguzo nne ambazo ni kutokomeza mimba za utotoni, kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kuzuia ukatili wa kimwili, kingono, na kisaikolojia pamoja na kuhakikisha watoto wa Kike na Kiume wanabaki shuleni.

Aidha ameendelea kufafanua kuwa Shirika la Plan International kwa kushirikiana na Serikali ya Canada chini ya mradi wa KAGIS limetoa vifaa hivyo ili kuisaidia sekta ya Elimu ambayo imekuwa na changamoto mbalimbali kama vile upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia na umbali kutoka nyumbani hadi shuleni hasa kwa shule za Sekondari.  Loyce Andrea Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mkoani amesema kuwa wanashukuru sana kwa kupata vitabu hivyo ambavyo vitawasaidia kujisomea wakiwa shuleni na hata majumbani huku akieleza kuwa wanaweza kufaulu vizuri kwa kusoma vitabu hivyo kwa kuwa mara zote majibu ya maswali mbalimbali yanayotolewa katika mitihani yao yanapatikana katika vitabu hivyo yakiwa na ufafanuzi wa kutosha.

Kupitia mradi huu wa KAGIS  chini ya ufadhili wa Serikali ya Canada shirika hilo linampango wa kujenga vyoo 50 katika shule za mradi katika mikoa ya Geita na Kigoma huku baiskeli 2,200 zikisambazwa kwa watoto wa kike wanaolazimika kutembea umbali mrefu kwenda shule sambamba na kutoa Elimu ya Afya ya uzazi na usawa wa kijinsia.




Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa