• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MWENGE WA UHURU 2023 WAPITISHA MIRADI YOTE 11 ILIYOKAGUA HALMASHAURI YA WILAYA GEITA.

Posted on: August 5th, 2023

Na. Agrey Singo.

Mwenge wa uhuru mwaka 2023 imepitisha miradi yote 11 yenye thamani ya shilingi 6,262,035,208 (bilioni 2.62) iliyotembelea na kukagua katika halmashauri ya wilaya ya Geita, Agosti 04, 2023.

Akizungumza katika katika uwanja wa shule ya msingi Ludete ambako mwenge wa uhuru ulilala mara baada ya kukamilisha kutembelea na kukagua miradi hiyo, kiongozi wa mbio hizo za mwenge kwa mwaka 2023 kitaifa, Ndugu Abdalla Shaib Kaim ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Geita kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwa kukidhi viwango vinavyotakiwa na kuwa na nyaraka zote.

Baada ya kuwasili halmashauri ya wilaya ya Geita, mwenge wa uhuru ulitembelea na kukagua mradi wa sekta ya mazingira wa shamba la miti linalomilikiwa na Ndugu Paul Dennis Kamando katika kijiji cha Nyamilyango, mradi wenye thamani ya shilingi 23,340,000.

Aidha, mwenge wa uhuru ulikagua na kuzindua jingo la utawala katika shule ya sekondari Kasota, jingo lenye thamani ya shilingi 102,850,000 likijengwa na Mgodi wa Geita Gold Mine Limited (GGML) kama uwajibikaji wa kampuni kwa jamii (Corporate Social Responsibility- CSR).

Aidha, mwenge wa uhuru 2023, ulisimama na kutoa ujumbe wa mwenge kwa wananchi waliojitokeza kwa wingi katika kijiji cha Saragulwa na kisha kwenda kugawa vyandarua 100 kwa wananchi katika zahanati ya Chigunga kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa malaria pamoja na kufanya usafi wa mazingira na upandaji miti katika zahanati hiyo.

Ukiwa katika shule ya sekondari Inyala, mwenge huo ulizindua klabu ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya sambamba na klabu ya kuzuia na kupambana na rushwa katika shule hiyo. Mwenge wa uhuru pia ukiwa katika kijiji hicho cha Inyala, uliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wenye thamani ya shilingi 463,975,432 unaotelekewa na  Wakala wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA.

Pia, mwenge ulitembelea mradi wa kufuga kuku unaomilikiwa na kikundi cha kuku farm uliopo Nyamigota wenye thamani ya shilingi 6,000,000, kikundi hicho kimekopeshwa na halmashauri ya wilaya Geita kupitia kitengo cha maendeleo ya jamii.

Baada ya hapo mwenge wa uhuru 2023, ulitembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya wilaya Katoro, mradi wenye thamani ya shilingi 3,200,000,000 ambapo kiongozi wa mwenge Ndugu Abdalla Shaib Kaim alotoa maelekezo machache ya kufanyia kazi kwa ajili ya kuboresha hospitali hiyo.

Mwenge wa uhuru ulimebelea na kukagua mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Katoro, Mradi wenye thamani ya shilingi 1,889,669,776 unaotekelezwa na Mgodi wa Geita Gold Mine Limited (GGML) kama uwajibikaji wa kampuni kwa jamii (Corporate Social Responsibility- CSR) ambapo kiongozi wa mbio hizo za mwenge kwa mwaka 2023 kitaifa, Ndugu Abdalla Shaib Kaim alitoa maelekezo kwa ajili ya uboreshaji.

Mwenge wa uhuru mwaka wa 2023, ulitembelea, kukagua na kuzindua ofisi ya kata Ludete, mradi uliogharimu shilingi 68,000,000 ambapo baadaye ukamilizia kwa kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya lami nyepesi CCM Katoro – Hospitali ya WIilaya kilomita 0.8 (mita 800) mradi unaotekelezwa na Wakala wa Barabara Vijijini Na Mijini- TARURA.

Baada ya mwenge kukamilisha shughuli ya kuembelea, kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi hiyo 11, akiwa katika uwanja wa shule ya msingi kiongozi wa mbio hizo za mwenge kwa mwaka 2023 kitaifa, Ndugu Abdalla Shaib Kaim aliipongeza halmashauri ya wilaya ya Geita kwa utekelezaji na usimamizi mzuri wa miradi yote ya maendeleo yanayotekelezwa, na kusema kuwa imekidhi viwango na nyaraka zote zilizotakiwa zilikwepo.

Kwa upande wake, mkuu wa wilaya ya Geita, Cornel Magembe aliwapongeza na kuwashukuru watumishi na wananchi wote wa halmashauri ya wilaya Geita wakiongozwa na mkurugenzi mtendaji Karia Magaro kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha katika kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na viwango stahiki.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa