• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU TARAFA YA BUTUNDWE-DC KOMBA

Posted on: March 11th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, ameanza ziara yake katika Tarafa ya Butundwe leo Machi 11, 2025, akiongozana na viongozi na wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi.

Mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba akizungumza katika mkutano wa hadhara katika kata ya Butundwe.

Katika ziara hiyo, Mhe. Komba ametembelea miradi ya afya, elimu na miundombinu, ikiwemo ujenzi wa Zahanati ya Nyandago, Zahanati ya Lukumbo, nyumba za walimu katika Shule ya Msingi Lukumbo na Jengo la Mama na Mtoto katika Zahanati ya Kasangwa. Ameelekeza miradi hiyo ikamilishwe kwa wakati ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Aidha, katika mkutano wa hadhara uliofanyika Butundwe, Mhe. Komba amesisitiza ushirikiano wa jamii katika kulinda usalama, akihimiza dhana ya Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi. Pia, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kusajili au kurekebisha taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.


Mkuu wa Wilaya ameonya dhidi ya vitendo vya ukatili kwa watoto wa kike na kuwataka wazazi kuhakikisha wanapata elimu bila vikwazo. “Mtoto wa kike atalindwa, atapewa elimu na hatokatishwa ndoto zake,” amesisitiza.

Kwa upande wa miundombinu, Mhandisi wa TARURA Wilaya ya Geita, Saimon Buganga, amesema zaidi ya Shilingi bilioni 1 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara, huku milioni 491 zikielekezwa kwenye ujenzi wa Barabara ya Chemamba-Kasamwa-Nyandago yenye urefu wa kilomita 18.


Miongoni mwa changamoto zilizowasilishwa na wananchi ni uhaba wa maji, mmomonyoko wa maadili, migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, pamoja na uwepo wa wanyamapori hatarishi. Mhe. Komba ameahidi kushughulikia changamoto hizo kwa kushirikiana na mamlaka husika.

Ziara hiyo inaendelea kesho kwa ukaguzi wa miradi mingine katika maeneo tofauti ya Tarafa ya Butundwe.




Matukio kwa picha ziara ya Mkuu wa Wilaya katika Kata ya Butundwe

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa