• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA WA GEITA AZINDUA WIKI YA MAZINGIRA KANDA YA ZIWA KWA NIABA YA WAZIRI MKUU

Posted on: June 1st, 2024

Mikoa 7 ya Tanzania imetakiwa  kuchukua hatua za kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaofanywa kwenye mikoa hiyo ili kurudisha uoto wa asili uliopotea.

Ndg Karia Rajabu Magaro, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya Geita, akifyeka nyasi wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani, yaliyofanyika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato Leo Juni Mosi, 2024.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais  Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa wito huo kwa mikoa hiyo wakati akiwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato  sehemu lilipofanyika zoezi la kupanda miti pamoja na kufanya usafi wa mazingira Kimkoa ikiwa ni kuelekea siku ya mazingira duniani.

Mhandisi Cyprian Luhemeja, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, wa pili kushoto aliyevaa shati la maua maua akiwa amesimimama pamoja na Mkuu wa Mkoa Geita Mhe Martine Shigela aliyesimama katikti aliyevaa track suti na kofia nyeusi pamoja na viongozi wengine, wakijiandaa kuhutubia wananchi kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani Leo Juni mosi, 2024.

Mhandisi Luhemeja ametaja mikoa inayotakiwa kuchukua hatua za kukabiliana na uharibifu wa mazingira ili kurudisha uoto wa asili uliopotea ni pamoja na Mwanza, Simiyu, Geita, Shinyanga, Tabora,Singida na Kigoma.

Mhandisi Luhemeja amesema kuwa kama mikoa hiyo haitachukua hatua ya kukabiliana na suala hilo kuna athari kubwa ya mazingira itakayopatikana kwa vizazi vijavyo.

“Kama hatutafanya jambo lolote sasa, miaka 20 ijayo watoto wetu watanung’unika sana, na tusidanganyane na maji ya ziwa Victoria pamoja na kuwa yapo jirani,  kuyasambaza ni kazi ngumu sana.

Nilipokuwa Wizara ya maji nilitembelea wilayani Bukombe, pale Bukombe nilikuta hata kuchimba maji ya chini ni shughuli maji yapo mbali sana, lakini hii ni kutokana na kuharibu mazingira hivyo tuanze mipango ya kuanza kuandika miradi ya kurudisha uoto wa asili hali siyo nzuri ’’ameongeza Luhemeja.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela akizungumza kwa niaba ya Mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kasimu Majaliwa Majaliwa (MB) amewataka wananchi wanaoshughulika na uchimbaji wa madini kurejesha uoto wa asili kwenye maeneo wanayofanyia kazi zao mara tu wanapomaliza shughuli za uchimbaji.

Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Geita Mhe Martine Shigela katika zoezi la kufanya usafi wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yaliyofanyika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato Juni Mosi, 2024.

Aidha amewataka Wananchi wote kuendelea kuona zoezi la kuyatunza mazingira kuwa endelevu kuanzia maeneo wanayoishi na sio jambo la siku moja tuu.

Wakati huo huo Mbunge wa Jimbo la Chato Mhe Medard Kalemani amesema kuwa wananchi wa Chato wataendelea kushirikiana na serikali  ili kutunza mazingira kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.

Mbunge wa jimbo la Chato Mhe Dkt Medard Kalemani aliyevaa shati jeupe, akipunga mkono wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yaliyofanyika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato Juni Mosi 2024

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Watumishi wa umma kutoka Wilaya za Mkoa wa Geita, Viongozi wa dini, vyama vya siasa na wananchi mkoani Geita.

Kila ifikapo June 5 ya kila mwaka dunia huadhimisha siku ya mazingira duniani lengo likiwa ni  kuhamasisha jamii kuelewa masuala ya mazingira na kuifanya jamii kuwa mstari wa mbele kuchukua hatua za kuhifadhi na kulinda mazingira.

Kauli mbiu ya mwaka huu katika wiki ya Mazingira Kitaifa na Kimataifa inasema "urejeshwaji wa ardhi iliyo haribiwa na ustahimilivu wa hali ya jangwa na ukame."

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa