• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MBIO ZA MWENGE WA UHURU GEITA DC

Posted on: October 9th, 2024

Mwenge wa Uhuru ni chombo kilichoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1961 ikiwa ni tunu na ishara ya kuwepo kwa Taifa huru la Tanganyika.

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilianza rasmi mwaka 1964 baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwenge wa uhuru umekuwa kichocheo kikubwa katika kuimarisha uhuru wa Taifa letu,umoja wa kitaifa, kudumisha amani, kulinda Muungano na kuhamasisha maendeleo ndani na nje ya taifa la Tanzania.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg Godfrey Eliakimu Mnzava wakisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba kwenye viwanja vya mapokezi ya Mwenge kata ya Bugulula Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Itakumbukwa kuwa tangu mwaka 1964 hadi 1992, mbio za Mwenge wa Uhuru zilikuwa zikiratibiwa na kusimamiwa kitaifa na chama cha Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP) na baadaye Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia Jumuiya zake za Umoja wa Vijana.

Huu ni mwaka wa 32 tangu mbio za Mwenge wa Uhuru zirejeshwe chini ya uratibu na usimamizi wa Serikali ambapo kwa mwaka 2024 Mwenge wa uhuru umebeba kauli yenye kuwahamasisha wananchi kujitokeza kushiriki uchaguzi wa serikali za Mitaa kwa amani na utulivu sambamba na kuendelea kushiriki kikamilifu katika harakati za kuhifadhi Mazingira kwa ujenzi endelevu wa Taifa chini ya kauli mbiu isemayo “Tunza mazingira nashiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa ujenzi wa Taifa endelevu”

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ndg Godfrey Eliakimu Mnzava akizindua Klabu ya kupinga na Kupambana na Rushwa shule ya sekondari Kasota

Aidha pamoja na kauli mbiu hii, Mbio za mwenge wa uhuru zitaendelea kuelimisha na kuihamasisha jamii ya watanzania kuhusu umuhimu na uzingatiaji wa lishe bora, mapambano dhidi ya rushwa, mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI, mapambano dhidi ya matumizi ya Dawa za Kulevya na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro akipanda mti kwenye shambala Miti lenye ukubwa wa Ekari 6 linalomilikiwa na Ndg George Patrick  Chomanga wakati wa mbio za mwenge wa Uhuru kama sehemu ya kuunga juhudi za Serikali katika utunzaji wa mazingira

Mwenge wa Uhuru 2024 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita umekimbizwa umbali wa 45.6 km kutoka eneo la Mapokezi hadi eneo la Mkesha na 30 km kutoka eneo la Mkesha hadi eneo  la Makabidhiano hivyo kukimbizwa kwa jumla ya 75.6 km ambapo jumla ya miradi 14 yenye thamani ya jumla ya Tsh 2,898,164,073.58 inayohusisha miradi ya Maendeleo, Malaria, Lishe pamoja na Klabu za wapinga Rushwa na Madawa na Kulevya imetembelewa ikiwa ni pamoja Kuzindua, kuona,pamoja na kuweka mawe ya Msingi katika Miradi mbalimbali na baadaye kukabidhiwa  Wilaya ya Sengerema Halmashauri ya Bushosa katika katika kijiji cha Nyamadoke Oktoba 6,2024.

Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg Godfrey Eliakimu Mnzava akipanda mti kwenye shambala Miti lenye ukubwa wa Ekari 6 linalomilikiwa na Ndg George Patrick  Chomanga wakati wa mbio za mwenge wa Uhuru kama sehemu ya kuunga juhudi za Serikali katika utunzaji wa mazingira

Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mji wa Geita (Kushoto) Yefred Miyenzi wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Oktoba 5, 2024 katika kata ya Bugulula


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa