• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAAFISA HABARI NI KIUNGO MUHIMU KATIKA KUIUNGANISHA SERIKALI NA WANANCHI-DKT MPANGO

Posted on: February 21st, 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdor Mpango leo Februari 21,2025 amefunga Mkutano wa 109 wa wadau wa elimu kwa umma unaofanyika Jijini Mbeya.

Mkutano huo ulifunguliwa February 18,2025  na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe Methusela Ntonda kwa niaba ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi.

Akizungumza katika Mkutano huo Mhe Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango amewaeleza washitiri hao kuwa wao ni kiungo muhimu katika kuunganisha Serikali na wananchi kwa kuzitumia kalamu zao vizuri.

Vilevile Dkt Mpango amesema agenda ya matumizi ya nishati safi ni agenda ya Taifa kwani inatoa msukumo wa kuunga mkono mkakati wa Taifa unaolenga Asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ifikapo mwaka 2034.

Pamoja na hayo Dkt Mpango amesema Serikali imesaini makubaliano ya awali ya Kiasi cha Bilioni 8.4 na makampuni ya usambazaji wa nishati safi ili kupunguza gharama za matumizi ya nishati safi kwa wananchi  katika kuendelea  kuhamasisha matumizi ya nishati safi.

Aidha Dkt Mpango  amewaeleza washitiri hao kuwa wanalo jukumu la kuhamasisha wananchi juu ya utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi.

Pamoja na hayo Dkt Mpango amewataka Maafisa Habari, Mahusiano na Mawasiliano kutoka Serikalini kuendelea kuwa daraja  linaloiunganisha  Serikali na wananchi kwa kutoa taarifa za mafanikio makubwa ya serikali.

" Nyie ni daraja linalounganisha serikali na wananchi hivyo mtoe taarifa kwa usahihi  ziwafikie  wananchi ili kuendelea kutunza amani na utulivu" Amesema Mhe Dkt Mpango.

Naye  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi amewataka Maafisa Habari na mahusiano na Mawasiliano kutoka Serikalini kuendelea kuyauza yale mazuri yote Serikalini inayoyatekeleza katika Taasisi zao.

" Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya kimkakati ikiwepo Bwawa la Nyerere, Reli ya Kisasa (SGR), Daraja la Kigongo Busisi ambalo ni la sita kwa Urefu Afrika, pamoja na miradi mingine ya Maendeleo" Amesema Profesa Kabudi.

Aidha Profesa Kabudi ametoa wito kwa Taasisi mbalimbali kuendelea kulitumia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kutangaza miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt Ayub Rioba Chacha ametoa shukrani zake kwa Washitiri wa Mkutano huo na kusema jumla ya Washitiri 280 wamehudhuria Mkutano huo.

Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwepo Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali,  Wakuu wa Mikoa ya Dodoma, Njombe, Songwe, Ruvuma, Wakuu wa Wilaya , Makatibu Tawala,  Wakurugenzi wa Taasisi mbalimbali na viongozi wa Chama na Dini.

Mkutano wa 109 wa wadau wa elimu kwa umma umefungwa rasmi Februari 21,2025 huku ukibeba kauli mbiu isemayo Tumia Nishati Safi, Tunza Mazingira.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa