• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

KAZUNGU: TUENDELEE KUHAMASISHA SUALA LA ELIMU KWENYE WILAYA YETU

Posted on: February 19th, 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Mh. Charles Kazungu, amewataka Wazazi Wilayani Geita kuhakikisha wanawaandikisha watoto wao waliofanikiwa kuchaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza kwa mwaka wa 2025 katika shule ambazo zinaendelea kujengwa katika Wilaya ya Geita.

Akizungumza hii leo kwenye Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani kwa kipindi cha Robo ya Pili 2024/2025 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya, Mh. Kazungu ametoa maelekezo kwa madiwani kuweka msisitizo kwa wazazi kuhakikisha wanaipa Elimu kipaumbele badala ya kuwatelekeza watoto wakizagaa mitaani.

"Sisi kama madiwani tuna jukumu la kuwahamasisha wazazi wawapeleke watoto shuleni kidato cha kwanza. Hii itasaidia kuondokana na tatizo la kukithiri kwa watoto waliopo mitaani." Amesema Mh. Kazungu.

Jumla ya wanafunzi 13,515 waliofaulu mtihani wa kumaliza Elimu Msingi mwaka 2024, wameweza kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza Kwa mwaka 2025, huku 95 kati yao walochaguliwa kwenda shule za Bweni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Geita, Mh. Charles Kazungu amewataka Madiwani  kuwahimiza Wazazi kuwapeleka shule watoto waliofanikiwa kujiunga na Kidato cha Kwanza.

Aidha, Halmashauri kupitia Divisheni ya Elimu Sekondari imeweza kufanya maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza kwa kuainisha mahitaji ya vyumba vya madarasa 293, pamoja na viti na meza 13,420.

Kwenye mkutano huo ulioingia siku ya pili, kamati zilizowasilisha taarifa ni pamoja na Kamati ya Fedha, Kamati ya Uongozi na Mipango, Kamati ya Uchumi, Kamati ya Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Elimu, Afya na Maji, Kamati ya kudhibiti UKIMWI, pamoja na Kamati ya Maadili.

Hali ya Ukusanyaji wa Mapato na Matumizi wa Halmashauri.

Hadi kufikia mwezi Disemba 2024, Halmashauri imeweza kukusanya kiasi cha Shillingi 520,508,095.24 na hivyo kufanikiwa kuvuka lengo la makisio iliyojiwekea.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya, Ndg. Karia Magaro ameweza kuipongoze timu ya mapato na kuishauri kuongeza bidii kwenye kasma ambazo bado hazijafikiwa,  huku pia akitoa rai kwa madiwani kuweza kuendelea kuisimamia miradi ya kimaendeleo na yenye tija kwa wananchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndg. Karia Magaro amesema kasi inatakiwa kuongezeka kwenye ukusanyaji wa Mapato ili kuhakikisha Halmashauri inafikia malengo iliyojiwekea.

Maelekezo ya Mkuu wa Wilaya kwa Halmashauri.

Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Geita, Ndg. Hashim Komba, Katibu Tawala wa Wilaya, Bi Lucy Beda amesema kuwa fedha kiasi cha Shilingi 100,000,000 zilizokuwa zimetengwa kwaajili ya miundombinu ya viti na meza, ziwezeze kutolewa kwa haraka kwakuwa shule zimeshafunguliwa.

Katibu Tawala wa Wilaya, Geita, Bi. Lucy Beda ameiagizia Halmashauri kuhakikisha inatoa fedha ili kuwezesha utoaji wa meza na madawati mashuleni.

Bi. Lucy Beda pia hakusita kutoa pongezi kwa Halmashauri kupitia kwa Mkurugenzi kwa kuweza kusimamia  utoaji wa mikopo kiasi cha Shilingi 689,000,000 kwa vikundi vya Wanawake, Walemavu na Vijana ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kuwataka Madiwani kuwahamasisha Vijana kwa kuchangamkia fursa hiyo.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Geita, Mhandisi Sande Batakanwa akichagia hoja ya Madiwani juu ya ufikishaji wa huduma ya maji karibu na wananchi, zoezi ambalo lipo katika hatua za mwisho kukamilika.


Meneja wa TARURA, Mhandisi Jerry Mwakapemba akiwasilisha mada kuhusiana na uendelezwaji wa ujenzi wa barabara mbalimbali katika Wilaya ya Geita.

Wenyeviti wa Kamati tofauti za Halmashauri wakiwasilisha taarifa za bajeti za Kamati wanazozisimamia kwa kipindi cha Robo ya Pili ya mwaka wa Fedha 2024/2025.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa