• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita Lamaliza kikao chake na kupitisha Taarifa ya Utendaji kazi kwa Robo ya Kwanza (Julai-Septemba 2023) ya Mwaka wa Fedha 2023/24

Posted on: November 16th, 2023

Na:Hendrick Msangi

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Geita  limefanya mkutano wake Novemba 15 na 16 ,2023  wa Robo ya Kwanza ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 (Julai – Septemba 2023) katika ukumbi wa mikutano wa Halmashuri hiyo iliyopo Kata ya Nzera wilayani Geita na kupitisha taarifa ya utendaji kazi kwa robo hiyo kwa kata zote 37 za Halmashauri hiyo.

Kikao hicho kilichofanyika kwa siku mbili kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali pamoja na wakuu wa idara mbalimbali katika Halmashauri hiyo chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Charles Kazungu ambaye pia ni diwani wa kata ya Butobela.

Aidha, katika kikao hicho ambacho siku ya kwanza kilianza na uwasilishwaji wa taarifa za utekelazaji wa shughuli za maendeleo ngazi ya kata kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2023 na siku ya pili kwa Wenyeviti wa Kamati za kudumu za Halmashauri kuwasilisha taarifa za kamati zao na wajumbe wa Baraza la Madiwani kuzipokea na kuzipitisha kwa pamoja.

Awali akifungua Kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo aliwataka waheshimiwa madiwani kusikiliza na kuuliza maswali au kutoa maoni na ushauri katika taarifa hizo ambazo ziliwasilishwa.

Akizungumza katika baraza hilo Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Geita Cornel Maghembe aliwapongeza madiwani hao pamoja na watumishi wa Halmashauri hiyo  kwa utendaji mzuri katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuendelea kusimamia vizuri shughuli zote za Halmashauri . Pamoja na hayo aliwaagiza Madiwani  hao kukaa kwa pamoja na kuona namna ya kutatua migogoro inayojitokeza kwenye vijiji na kata zao ili wananchi waendelee kuwa na Imani na serikali yao inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akiendelea kutoa hotuba yake, aliziagiza Taasisi za TARURA na RUWASA ambazo zinagusa wananchi moja kwa moja kuhakikisha wanatatua changamoto kwa wananchi

Nayo kamati ya Siasa ya Wilaya ilisema imeridhika na shughulizi za utendaji katika Halmashauri hiyo na kuitaka Halmashauri kuendelea kuwasaidia Madiwani kuzitatua changamoto zilizodumu kwa muda mrefu kwa wananchi ikiwepo migogoro katika kata zao.

Pia ilitoa maelekezo kwa Wakala wa barabara za vijijini na mijini (TARURA) kuwa na mpango wa muda mrefu hasa kwa barabara zenye changamoto. “Wekeni mipango ya muda mrefu kwa barabara zinazohitaji dharura badala ya kusubiri mpango wa bajeti 2023/24” alisema Cde. Barnabas Mapande ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita.

Kamati hiyo pia iliagiza kero ya kutokuwepo kwa walimu wa jinsi ya kike kwenye baadhi ya shule itatuliwe mapema ikiwa ni pamoja na kuwaajiri walimu wa muda mfupi wakati serikali ikiwa kwenye mpango wa kuleta walimu wa kudumu katika shule hizo ili kupunguza utoro kwani kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na afisa elimu msingi Mwalimu Ibrahimu Bunangoi wa halmashauri hiyo,ilisema Halmashauri inahitaji walimu 6416 na kwa sasa idadi ya walimu  shule za msingi ni walimu 3102.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya Wilaya ya Geita Bi. Sara Yohana amelishukuru baraza kwa pongezi na kuwaahidi waheshimiwa madiwani kuwa Halmashauri  itaendelea  kufanya kazi kwa bidii na kwa kushirikiana na Madiwani hao ikiwa ni pamoja na kufuata maelekezo ya kiutendaji  yaliyotolewa na baraza hilo

Akifunga kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu  amewashukuru Waheshimiwa Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kushiriki katika baraza hilo huku akiwataka kuendelea kutekeleza yote ambayo yamejadiliwa  ili kutimiza azma ya chama na serikali  kwa wananchi.” Uadilifu ndio msingi mkubwa wa utumishi wa umma “alisema Mhe. Kazungu akifunga kikao hicho cha baraza la madiwani robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2023/24 la Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa