• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAZEE WA GEITA WAWAASA VIJANA KUACHA TABIA ZA KUILALAMIKIA SERIKALI

Posted on: December 10th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba ameongoza mamia ya Wananchi Mkoani  Geita Katika Maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika ukumbi wa GEDEKO Mkoani Geita Disemba 9, 2024.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Geita Ndg Herman Matemu alisema Uhuru wa Tanzania haukupatikana kirahisi bali ulikuwa ni mchakato wa muda mrefu na kuwataka wananchi kuendelea kuwa enzi waasisi wa Uhuru. “Tupo huru na maendeleo yanafanyika hivyo tuendelee kuwa na jukumu la ku enzi viongozi wetu waliomwaga damu kuipambania nchi yetu” Amesema Mtemu

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba akizungumza mbele ya wageni waalikwa na wananchi katika hafla ya maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru.

Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela, Mhe Komba katika hotuba yake amezungumza na wazee ambao walikuwepo kabla ya Uhuru ili kuwaelezea wananchi waliohudhuria katika  kongamano hilo hali ilivyokuwa kabla ya uhuru na hali ilivyo kwa sasa katika Serikali.

Wakizungumza wakati wa Maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru yaliyofanyika katika Ukumbi wa GEDEKO Mkoani Geita  wazee hao wamesema miaka ya nyuma kabla ya Uhuru Geita wakati huo ikiwa ni Wilaya haikuwa na huduma za kijamii kama shule na hospitali na badala yake walilazimika kwenda Mwanza ila kwa sasa Serikali Inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya kazi njema zilizo asisiwa na waasisi na katika kusherehekea miaka 63 ya Uhuru kila kata ina shule, zahanati na vituo vya afya ni vingi.

Wazee mbalimbali wa umri wa zaidi ya miaka 63 wakizungumza mbele ya kongamano, tofauti ya kimaendeleo iliyopo mara baada ya Uhuru wa Tanzania bara, na sasa

Aidha wazee hao wamewataka vijana kuacha kuilalamikia serikali kwamba haileti maendeleo kwenye jamii zao badala yake waiunge mkono izidi kuleta maendeleo kwani mpaka sasa Tanzania imepiga hatua kubwa ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali

Pamoja na hayo Mhe Komba ametoa rai kwa wananchi kuendelea kuwa wazalendo, kujituma, kuendelea kufanya kazi kwa bidii  kwani miaka 63 ya uhuru imekuwa na ushindi katika sekta mbalimbali za maendeleo.” Mimi na wewe tujiulize tunafanya nini, tuendelee kuwa na tafakari ya kina tumetoka wapi na tunaenda wapi” amesema Kaimu Mkuu wa Mkoa Mhe Komba.


Katika Maadhimisho hayo mada mbalimbali ziliwasilishwa katika kuulezea umma namna ambavyo Taifa lilipitia michakato mbalimbali katika Kupata Uhuru.

Kwa upande wake Mwalimu Isdory Vitus Kalimuwabu kutoka shule ya Sekondari Mwatulole alizungumzia mada ya Historia ya harakati za kupata Uhuru wa TanzaniaBara na Mchango wa Viongozi wa Taifa katika maendeleo ya kiuchumi Tanzania na kuelezea hatua mbalimbali zilizopitiwa hadi kupata uhuru.

Mada nyingine iliyozungumziwa katika Kongamano hilo ni Tanzania na harakati za Mapinduzi ya Kiuchumi katika Sekta  za elimu, afya, Maendeleo ya jamii, Kilimo, Miundombinu,Nishati, biashara, mawasiliano na ujenzi iliyo wasilishwa na Ndg ALLY Abuu Kutoka chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT).

Pamoja na mada hizo, Ndg Kadole Ngumungu ambaye ni Afisa Utumishi na Rasilimali watu Halmashauri ya Mji Geita aliwasilisha mada isemayo Hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ukuaji wa siasa na maendeleo ya Taifa  huku Afisa Maendeleo ya Vijana Mwandamizi Ndg Zengo Polle akiwasilisha mada ya Uhuru na maadili ya Taifa katika kuchochea fikra za kizalendo na masuala ya uongozi kwa vijana.

Maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru mwaka huu yamebebwa na Kauli mbiu isemayo, “Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara: “UONGOZI MADHUBUTI NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI NI MSINGI WA MAENDELEO YETU.”

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa