• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI WAASWA KUZINGATIA UTUMIAJI WA LISHE BORA KATIKA MAKUZI YA WATOTO

Posted on: August 7th, 2024

WAZAZI nchini wameaswa kuzingatia lishe bora ili kuwezesha upatikanaji wa maziwa ya kutosha na yenye ubora pindi wanapowanyonyesha watoto wachanga ili kusudi waweze kuwa na afya bora.

Hayo yamesemwa Agosti 07, 2024 na Afisa Lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Bi Umi Zuberi Kileo katika maadhimisho ya kilele cha wiki ya unyonyeshaji Maziwa ya Mama pamoja na kutoa elimu ya uzazi salama yaliyofanyika katika Zahanati ya Kata ya Lwezera ambapo amewasisitiza akina mama kuhakikisha wanapata lishe bora muda wote ambao wanakua katika kipindi cha unyonyeshaji wa mtoto.

Bi Umi Kileo ambeye ni Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita akielezea umuhimu wa lishe bora kwa mama anaye nyonyesha ambapo amewataka wazazi kuzingatia lishe iliyo bora ili kusudi waweze kutoa maziwa yenye ubora na ambayo hayataweza kumletea madhara ya kiafya mtoto mchanga.

"Mzazi anapaswa azingatie kua anapata lishe iliyo bora ili kusudi aweze kutoa maziwa yenye ubora na ambayo hayataweza kumletea madhara yeyote ya kiafya mtoto mchanga.”Amesema Bi Umi.

Aidha Afisa Lishe huyo amewaeleza wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo kuwa maziwa ya mama yanasaidia kumpa kinga madhubuti mtoto pindi anapokua amezaliwa na mama anapaswa kumyonyesha kwa angalau miezi sita pasipo kumpa kitu kingine.

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakifuatilia masomo ya lishe bora kwa wazazi wakati wa maadhimisho ya kilele cha wiki ya unyonyeshaji Maziwa ya Mama duniani ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita yamefanyika kata ya Lwezera.

Pamoja na hayo Bi Umi amewasihi akina mama kuendelea kuwanyonyesha watoto kwani kwa kufanya hivyo wataendelea kuboresha afya zao.

Kwa upande wake, Bi Theresia Simon ambae ni Afisa Muuguzi, ameishukuru Halmashauri ya Wilaya kwa kupitia Wizara ya Afya, kuandaa programu hiyo pamoja na kuitaka iwe endelevu kwa kuwa akina mama wanaojifungua ni wengi.

"Huduma hii ikiwa endelevu itaendelea kuleta muitikio kwa akina mama kwa kuwa kila mwezi wamama wanajifungua.” Amesema Bi Theresia huku akishukuru kwa somo zuri lililotolewa juu ya lishe bora.

Maafisa Lishe wakiwaonyesha wananchi waliohudhuria maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji kata la Lwezera namna ya kuandaa uji bora wa lishe. Wazazi wameshukuru kwa mafunzo hayo ya uandaaji wa lishe bora na umuhimu wa mama kunyonyesha mtoto na kuomba somo hilo liwe endelevu kuwasaidia akina mama wanaojifungua kila mwezi

Wakati huo huo Bi Janet Jackson kwa niaba ya akina mama waliojitokeza kwenye program hiyo ameiomba serikali iweze kuwaelimisha zaidi wananchi haswa wanaoishi vijijini ili kuwa na jamii yenye ustawi na afya bora.

"Tunashukuru kwa elimu hii tulioletewa na wahudumu wetu wa afya. Wito ni kuiomba serikali iweze kutoa huduma hii sehemu tofauti tofauti haswa huku sehemu za vijijini ili sote tuwe na afya njema na hili kwa kiasi kikubwa litasaidia kuwa na jamii yenye afya njema. " Amesema Bi Janet.

Wiki ya Unyonyeshaji Maziwa ya Mama huadhimishwa duniani kote kuazia tareh 1-7 Agosti kila mwaka kwa lengo la kusisitiza umuhimu wa kulinda, kuimarisha na kuendeleza unyonyeshaji wa maziwa ya mama, ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ilikua ni, "TATUA CHANGAMOTO: SAIDIA UNYONYESHAJI WATOTO KWA WOTE."

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa