• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

Posted on: June 18th, 2025

Kufuatia maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma barani Afrika, Watumishi wa Umma kutoka sekta mbali mbali Mkoani Geita wamehimizwa kuwa wanajifanyia tathmini ili waweze kukidhi sifa za kupanda madaraja.

Akizungumza na Wakuu wa Idara kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita mapema wiki hii katika awamu ya pili ya utoaji wa mafunzo ya utumiaji wa mfumo wa kupima Uwajibikaji na Utendaji wa Watumishi (ESS), Mratibu kutoka Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ndg. Elibariki Funga, amewasisitiza Wakuu hao wa Idara kuwafanyia tathmini watumishi walio chini yao kwa kuwa ni muhimu ili kuweza kuwaweka kwenye nafasi ya kupanda madaraja pindi muda wa kupanda madaraja utakapowadia.

Aidha, Ndg. Funga pia ameongeza kwa kusema kuwa, lengo kuu la kufanya tathmini miongoni mwa watumishi ni pamoja na kuhakikisha Watumishi wanatekeleza wajibu wao na hivyo wanapaswa kulichukulia jambo hilo kwa uzito mkubwa.

“Kila mtumishi anatakiwa awe na majukumu yake mwenyewe. Hivyo lazima uwepo mpango madhubuti, ndani ya muda husika wa kufanya tahmini kwa Watumishi wa Umma. Tunapaswa kutambua kuwa tunajenga cha kwetu.”

Kwa upande mwingine, Ndg. Raphael Kimaro (Mratibu kutoka Ofisi ya Raisi Menejienti ya Utuishi wa Umma na Utawala Bora) amesema kuwa, nia ya mafunzo hayo ni kuhakikisha yanaleta Utumishi nwenye tija pamoja na kujengeana uwezo ndani ya taasisi husika.

Kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Mkuu wa idara ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (M) Ndg. Herman Matemu amewataka Watumishi mkoani humo kujaza majukumu yenye uhalisia lakini pia kuwataka kutoa mrejesho kwa watumishi wanaowasimamia kwa wakati.

Siku ya Utumishi wa Umma husherehekewa Juni 23 kila mwaka na nchi wanachama wa Umoja Wa Afrika kwa kutambua mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao ambapo kwa mwaka huu iliongozwa na kauli mbiu isemayo: “Himiza matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji.”

Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TIMU YA MENEJIMENTI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YARIDHISHWA NA KASI YA UKAMILISHAJI WA MIRADI

    October 17, 2025
  • GEITA DC KUENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA BOOST YENYE THAMANI YA BILIONI 3.2

    October 09, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NYANG'WALE ATEMBELEA BANDA LA MAONESHO YA MADINI LA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

    September 24, 2025
  • WAUGUZI WA AFYA NA MAAFISA LISHE GEITA DC WAASWA KUEPUKA MIGOGORO MAENEO YA KAZI.

    September 22, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa