• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WAADHIMISHA KUMBUKUMBU YA SIKU YA MASHUJAA TANZANIA JULAI 25-GEITA DC

Posted on: July 25th, 2024

July 25 kila mwaka ni siku ya Historia kwa taifa la Tanzania ambapo huadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa katika kuwaenzi mashujaa ambao kwa uzalendo mkubwa na ujasiri wao waliweza kujitolea maisha yao kwa ajili ya taifa letu katika kupigania uhuru na kuilinda nchi yetu.

Tunapoadhimisha siku hii, tunatambua na kuthamini juhudi zao katika kuleta amani uhuru na maendeleo katika taifa letu. Siku ya mashujaa inatupa fursa ya kujifunza kutokana na historia yetu na kufahamu umuhimu wa kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajili yawengine.

Tunawaenzi mashujaa wetu  kwa matendo yetu ya kila siku kwa kufanya kazi kwa bidii, kufanya matendo ya kijamii ikiwa ni pamoja na kufanya usafii kwenye hospitali, nyumba za wazee, kupanda miti, kuendelea kuilinda amani na kushirikiana kwa hali na mali kwa maendeleo ya taifa letu.

Katika kuadhimisha siku hii muhimu kwa taifa letu, watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Ndg Karia Rajab Magaro leo Julai 25, 2024 wameshiriki zoezi la usafi katika hospitali ya Wilaya-Nzera pamoja na kupanda miti.

Mkurugenzi Mtendaji ndg Karia Rajab Magaro akipanda mti ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya mashujaa Tanzania ambapo kila mwaka huadhimishwa Julai 25.

Akizungumza na watumishi mara baada ya zoezi la usafi na upandaji miti, Ndg Karia amewataka watumishi  kuendelea kushirikiana kwa pamoja katika kuendeleza na kulinda urithi wa mashujaa wetu na kuhakikisha vizazi vijavyo vinaishi katika taifa lenye amani na ustawi ili waendelee kuwa na kumbukumbu ya mashujaa waliopiginania nchi yetu.

Mkurugenzi Mtendaji ndg Karia Rajab Magaro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Julai 25 katika siku ya kumbukumbu ya maadhimisho ya siku ya mashujaa Tanzania ambapo  siku hii ni katika kutambua na kuthamini juhudi za Mashujaa katika kuleta amani uhuru na maendeleo katika taifa letu.

Aidha kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika  katika jiji la Dodoma ambapo mgeni rasmi ni Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa katika zoezi la usafi katika siku ya kumbukumbu ya maadhimisho ya siku ya mashujaa Tanzania.

Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Hendrick Msangi akipanda mti katika siku ya kumbukumbu ya maadhimisho ya siku ya mashujaa ambayo huadhimishwa kila mwaka Julai 25.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa