• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WA UMMA WASISITIZWA KUTUMIA MFUMO WA UNUNUZI WA UMMA NeST KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: August 30th, 2024

Nzera-Geita, Agosti 30, 2024

Kila  mwaka Serikali inatumia sehemu kubwa ya fedha zinazoidhinishwa  kwenye bajeti  za Mafungu mbalimbali kwa ajili ya ununuzi wa bidhaa, kandarasi za ujenzi na huduma kwa kuzingatia matakwa ya sheria ya ununuzi wa umma, SURA 410 na kanuni zake.

Aidha serikali imeendelea kudhibiti matumizi ya fedha  zinazopolekwa  kwenye kila fungu kwa kutumia njia mbalimbali ikiwepo  mifumo ya kielekroniki ili kuleta tija na ufanisi unaostahili katika utekelezaji wa bajeti ya fungu husika.

Mafunzo ya matumizi ya mfumo wa kielekroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) yameendelea kutolewa kila mara ili taasisi nunuzi zote ziweze kutumia mfumo wa NeST pamoja na watumishi wa umma wote wanaohusika na mchakato wa manunuzi ndani ya Taasisi kuwa na uwezo wa kutumia mfumo huo baada ya kuandaa bajeti sahihi inayo akisi ununuzi halisi unaofanyika kwa kila idara ndani ya taasisi hizo.

Katika kuhakikisha matumizi ya mfumo wa manunuzi wa NeST unatumiwa ipasavyo, Halmashauri ya Wilaya ya Geita kupitia Idara zake imeendelea kutoa mafunzo ili kuwajengea uwezo watumishi wa umma kufanya manunuzi kwa kutumia mfumo wa NeST.

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Sarah Yohana Yohana  amewataka watumishi wa umma kuzingatia kanuni za manunuzi ili fedha iliyoletwa na serikali iweze kukamilisha miradi lengwa na kwa wakati. Ameyasema hayo Agosti 30, 2024 akifungua mafunzo ya matumizi ya mfumo wa manunuzi wa umma NeST yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Awali akifungua mafunzo kwa watumishi wa umma wenye miradi katika maeneo yao ,Walimu Wakuu, Wahasibu wa shule na Maafisa elimu kata wa shule za msingi Ikigijo iliyopo kata ya Kakubilo  na Bwawani kata ya Ludete zilizopokea fedha za miradi Shilingi Milioni 348,500,000 kila moja, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Sarah Yohana  amewataka watumishi hao kuzingatia kanuni za manunuzi ili fedha iliyoletwa na serikali iweze kukamilisha miradi lengwa na kwa wakati.

Aidha Bi Sarah Yohana amewata watumishi hao kusimamia matumizi sahihi ya BOQ na kusisitiza manunuzi yote yazingatie bei ya soko na ubora wa vifaa kwa mujibu wa BOQ au makisio pamoja na kuwa na faili la mradi (Box file) ili kila nyaraka ya mradi ihifadhiwe kwa mpangilio ikiwemo mikataba watakayoingia na mafundi.

Watumishi wa umma ambao ni wasimamizi wa miradi katika maeneo yao ,Walimu Wakuu, Wahasibu wa shule na Maafisa elimu kata wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri wakati wa mafunzo ya mfumo wa manunuzi wa umma NeST. Katika mafunzo hayo wamesisitizwa kusimamia matumizi sahihi ya BOQ na kusisitiza manunuzi yote yazingatie bei ya soko na ubora wa vifaa kwa mujibu wa BOQ au makisio pamoja na kuwa na faili la mradi (Box file) ili kila nyaraka ya mradi ihifadhiwe kwa mpangilio ikiwemo mikataba watakayoingia na mafundi.

Kwa upande wake Mkuu wa divisheni ya elimu ya awali na msingi Mwl Paul Magubiki amewasisitiza walimu hao kuzingatia maelekezo yaliyotolewa  katika mafunzo hayo ili miradi iweze kukamilika kwa wakati na kuwataka kubainisha mapema changamoto watakazokuwa wanapitia na kuziwasilisha kwa  wakati ili taasisi iendelee kusimamia sheria za manunuzi na kuwataka kukubali mabadiliko ya kimfumo.

Jumla ya kiasi cha shilingi milioni 697,000,000 zimepokelewa kwa ajili ya miradi ya shule mbili za msingi ambazo ni Ikigijo iliyopo kata ya Kakubiro jumla ya shilingi 348,500,000 na shule ya msingi Bwawani kata ya Katoro shilingi 348,500,000.

Mkuu wa divisheni ya elimu ya awali na msingi Mwl Paul Magubiki amewasisitiza walimu wanaosimamia miradi katika maeneo yao  kuzingatia maelekezo yaliyotolewa  katika mafunzo ya mfumo wa manunuzi wa umma NeST ili miradi iweze kukamilika kwa wakati na kuwataka kubainisha mapema changamoto watakazokuwa wanapitia na kuziwasilisha kwa  wakati ili taasisi iendelee kusimamia sheria za manunuzi

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za miradi ya maendeleo katika kuwatumikia wananchi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa