• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WA UMMA WAASWA KUSIMAMIA KWA UADILIFU FEDHA ZA MAENDELEO –GEITA DC

Posted on: May 19th, 2024

Na: Hendrick Msangi

KAMENA MAY 19, 2024

Kazi imeendelea ikiwa ni operesheni ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi katika Kata 9 za awamu ya kwanza Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akiwa katika kata ya Kamena inayoongozwa na Diwani Mhe Peter Kurwa, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba amekagua miradi ya maendeleo ambayo ni zahanati, nyumba za watumishi na ujenzi wa shule katika vijiji vinne katika kata hiyo ambavyo ni Kamena, Nyashihima, Imalampaka na Ndelema.

Mhe Hashim Abdallah Komba wa kwanza kushoto, Mkuu wa Wilaya ya Geita akiwa na Kaimu Katibu Tawala Janet Mobe, pichani kulia, wakiwa wamebeba tofari  alipotembelea ujenzi wa Shule ya Sekondari yenye vyumba 3 vya madarasa Kijiji cha Ndelema kata ya Kamena nguvu za Wananchi ambapo alifanya harambee ndogo na kupatikana mifuko ya saruji 200 katika kuunga mkono juhudi za Wananchi.

Akimkaribisha katika kata hiyo, Mhe Winfrida Daudi Malunde ambaye ni diwani wa viti maalum na mlezi wa kata hiyo, amemuomba mkuu wa wilaya ya Geita, kupitia CSR kuweka mkazo miradi ya afya katika kata hiyo ili kuendelea kuwapunguzia wananchi umbali mrefu kupata huduma za afya. “Umeminiwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, tunaamini hakuna kazi itakayosimama, tunaomba kupitia Mgodi wa Dhahabu (GGML) fedha za CSR zikakamilishe miradi ili wananchi wapate huduma katika maeneo yao. Amesema Mhe Winfrida Malunde diwani mlezi wa kata ya Kemana

Kiongozi ni mfano. Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba amewataka Watumishi kuendelea kusimamia fedha za wananchi zinazokuja kwenye maeneo yao kwa uadilifu mkubwa sana, "sitavumilia kuona fedha za wananchi zinachezewa, hivyo mkasimamie fedha za miradi zinazokuja katika maeneo yenu”

Akihutubia Mkutano wa Hadhara katika kusikiliza kero za wananchi, Mhe Komba amesema hatovumilia kuona fedha za wananchi zikichezewa na miradi ikishindwa kukamilika na kuwataka watumishi wa umma kusimamia fedha ili miradi iende vizuri. “Endeleni kusimamia fedha za wananchi zinazokuja kwenye maeneo yenu kwa uadilifu mkubwa sana, sitavumilia kuona fedha za wananchi zinachezewa, hivyo mkasimamie fedha za miradi zinazokuja katika maeneo yenu” amesema Mhe Komba.

Aidha Mhe Komba  ametoa pongezi kwa jitihada zilizoanza kufanywa na mgodi wa dhahabu wa Geita (GGML) kupitia fedha za wajibu wa kampuni kwa jamii (CSR) kwa kupeleka  wakandarasi na kuanza haraka kwa ukamilishaji  wa mradi wa ujenzi wa vyumba sita vya madarasa katika shule ya msingi Kamenaikiwa ni siku chache  tangu alivyoitisha kikao na wadau hao katika kuweka makabaliano ya kukamilisha miradi  na kuwataka wale wote wanaohusika na miradi ya maendeleo kuacha uzembe ili wananchi wasiendelee kuteseka.

Ukamilishwaji wa Madarasa 7 shule ya Msingi Kamena unaotekelezwa na Kampuni ya Gesap Engineering Ltd.

Pamoja na hayo ameendelea kusisitiza uwepo wa madawati ya kusikiliza kero za wananchi kwa kushuka chini kusikiliza wananchi na sio kukaa ofisini. “Nimekuja mwenyewe kuonyesha mfano ili kusikiliza kero na changamoto za wananchi na nimeambatana na wataalam wa kada zote ili kuisogeza serikali jirani na wananchi

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa