• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WAPEWA MAAGIZO KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAO YA KILA SIKU GEITA DC

Posted on: March 17th, 2024

Na: Hendrick Msangi

Katika Kikao elekezi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kati ya Watendaji wa Kata na Vijiji pamoja na Timu ya Menejementi ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita , watendaji wa kata na vijiji wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi ili kuiletea Halmashauri sifa njema na kuinua mapato ya Halmashauri.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita yenye jumla ya kata 37 na vijiji 145 shughuli kubwa za uzalishaji zikiwa ni  kilimo, ufugaji, uvuvi uchimbaji madini na viwanda vidogo huifanya Halmashauri kupata mapato yake yake ya ndani kupitia shughulizi zinazofanyika ndani ya kata zote 37.

Ili kuendelea kusimamia vyanzo vya mapato na kuongeza pato la Halmashauri, watendaji wa kata na vijiji wametakiwa kujituma  na kuwatumikia wananchi katika maeneo yao ikiwa na ni pamoja na kuwa na njia nzuri za ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza na watendaji hao katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, Afisa Kilimo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Alphonce Bagambabyaki amewataka watendaji hao kuwahimiza  maafisa mifugo walio kwenye kata zao  kukusanya mapato ya ada ya ukaguzi  baada ya kukagua nyama ili kuendelea kuongeza mapato katika chanzo hicho.

Aidha kwa upande wa ushuru wa mazao ya samaki, watendaji hao walielekezwa kutoza ushuru kuanzia kilo moja ya samaki kwa shilingi 100 na kuwataka kuwajulisha maafisa uvuvi pindi wanapotaka kufanya doria za kwenye maji.”Ni kosa kwa watendaji kufanya doria kwenye maji bila kuwepo kwa Afisa Uvuvi” alisema Dkt Alphonce.

Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita walipozungumza na Watendaji wa Kata na Vijiji kuwapa maelekezo katika kuileta Halmashauri sifa njema katika utendaji kazi wao.

Pamoja na hayo watendaji hao wametakiwa kutokukata stakabadhi ya mazao ya kilimo bila kushuhudia gari lililobeba mazao ili kuepuka kukata ushuru pasipo kujiridhisha na kuwataka kuwepo kwa watu kwenye vizuizi (Barrier ) muda wote kwani asilimia Zaidi ya 70 ya mazao yanasafirishwa usiku na kutakiwa pia kukatiwa ushuru kwa mazao yote yanayosafirishwa na bodaboda au maguta kwa kuwa imebainika wengi hutumiwa na wafanyabiashara kusafirisha mazao hayo kutoka eneo moja kwenda lingine na kukwepa kulipa ushuru.

Kwa upande mwingine watendaji hao wametakiwa kuhakikisha wanafanya vikao vya kisheria, kusoma mapato na matumizi katika maeneo yao, kusimamia mahudhurio ya watumishi walio chini yao na kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo katika kata zao kwa kuzisimamia kamati za miradi kwani wao ni wadau wakubwa katika miradi inayoendelea kwenye kata zao hivyo kutakiwa kusimamia maboma yanayoanzishwa na wananchi yawe na ubora sawa na majengo ya serikali.

Watendaji wa Kata na Vijiji kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakipokea maelekezo kutoka kwa timu ya menejimenti ambapo wametakiwa kuwa waadilifu katika utendaji wao ili kuendelea kuinua mapato ya Halmashauri ikiwa ni mapoja na kusimamia miradi yote ya maendeleo katika maeneo yao.

Akiwapa maelekezo hayo Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dominic Shilingo amewataka watendaji hao kuwa na ushirikiano pale fedha za miradi zinapoingia kwenye kata zao, na kuhakikisha vifaa vya ujenzi vinakaguliwa ili kuwa na ubora unaostahili pamoja na kuzingatia thamani ya soko kuepuka kuweka maslahi mbele kwa fedha za serikali na kuwataka kuwashirikisha wananchi kushiriki katika miradi ya maendeleo katika maeneo yao. Aidha Mhandisi Shilingo aliwataka watendaji hao kufuatilia vibali vya ujenzi unaoendelea kwenye maeneo yao kwani ni chanzo cha mapato ya halmashauri.

Swala la lishe kwa wanafunzi nalo halikuachwa nyuma ambapo watendaji hao walitakiwa kulipa kipaumbele kwani ni agizo la serikali wanafunzi wapate lishe wawapo shuleni,

Akizungumza katika kikao elekezi hicho kwa niaba ya Mkuu wa Divisheni ya Elimu awali na msingi Mwalimu Neema Mwaluko alisema ofisi ya Mkurugenzi inaendelea kuwashukuru watendaji hao kwa kazi nzuri ya kuhamasisha swala la lishe shuleni kwani ongezeko la shule zinazotoa lishe kwenye halmashauri zimeongezeka kutoka shule 84 hadi shule 178 kati ya shule 235 za serikali na kuwataka kuendelea kuelimisha wazazi kuchangia chakula kwani ni agizo la serikali jamii ichangie ili watoto wapate chakula shuleni.

Watendaji wa kata  na Vijiji kwa pamoja wameazimia kutekeleza na kuyasimamia yote waliyoelekezwa na uongozi wa Halmashauri ili kuendelea kuipa sifa njema Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Aidha Mwl Neema aliwataka watendaji hao kuendelea kusimamia swala la utoro shuleni kwa kuweka mikakati ya kupunguza utoro kwani Halmashauri inakabiliwa na utoro mkubwa wa wanafunzi sawa na asilimia 11 kulinganisha na Halmashauri nyingine. Pamoja na hilo watendaji hao walitakiwa kusimamia swala la ulinzi na usalama kwenye shule kwani zipo baadhi ya shule kuvamiwa na wananchi. “Inasikitisha mahindi na vifaa vinaibiwa, wapo pia walimu ambao wanavamiwa na kuibiwa mali zao, mkaimarishe ulinzi kwa kuweka mikakati na kuepusha tabia hizo za uvamizi” alisema Mwl Neema.

Akifunga kikao hicho kwa niaba ya Mkuregenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Bi Sarah Yohana ambaye ni Mkuu wa Idara ya Mipango amewataka watendaji hao kutekeleza yote waliyoelekezwa na kuazimiwa ili kuendelea kuipa halmashauri sifa njema katika kuinua mapato.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa