• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WA VIJIJI WAPEWA SEMINA UTEKELEZAJI AFUA ZA LISHE-GEITA DC

Posted on: December 23rd, 2023

Na Hendrick Msangi

Katika kuhakikisha Halmashauri ya Wilaya ya Geita inafikia malengo katika utekelezaji wa afua mbalimbali za lishe, Watendaji wa Vijiji vya Halmashauri hiyo wameendelea kuhamasishwa kuwasaidia wananchi katika maeneo yao ili watekeleze afua hizo kwakuwa mabalozi wazuri kwa jamii inayowazunguka kutambua umuhimu wa lishe bora.

Hayo yameelezwa Desemba 18, 2023 wakati wa kikao cha Maafisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Watendaji wa Vijiji kujadili Mkataba wa Lishe katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo kata ya Nzera Wilayani Geita.

Awali akifungua semina hiyo elekezi Msimamizi Mkuu wa shughuli za afya, Lishe na Ustawii katika Jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Modest Buchard alisema jamii inapaswa kuwa na uelewa mpana kuhusu maswala ya Lishe ili kupunguza na kumaliza athari za utapiamlo katika jamii  ikiwa ni pamoja  na kuwataka watendaji hao kuwa mabalozi kwa kuhakikisha wanatoa elimu wanayoipata kwa kufuatilia huduma za afya na lishe kwa mama na mtoto kwa kuihamasisha jamii kushiriki  vema bila kuacha ushiriki wa baba katika maswala yote ya lishe kwa kuzingatia kunakuwepo na ulaji mzuri na wenye kuzingatia vyakula venye faida katika mwili


Naye Afisa Lishe Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Umi Zuberi  Kileo alisema kulingana na Mkataba wa lishe ambao kwa awamu ya tatu ulisainiwa Septemba 30,2022 baina ya Mhe Rais na wakuu wa Mikoa ulielekeza wajibu  kwa watendaji wote kwa kuhakikisha ajenda ya lishe inakuwa ya kudumu katika vikao vya Halmashauri ya kijiji, kuchochea na kuibua fursa za lishe ikiwa ni pamoja na kutatua matatizo ya lishe kwenye jamii zao kwa kuhakikisha shughuli za lishe zinatolewa taarifa pamoja na kuwatambua wadau wote kwenye ngazi ya kijiji.

Aidha Bi Umi aliendelea kusema , Mkataba huo unatoa wajibu kwa kijiji kukusanya, kutathmini na kujadili taarifa za lishe kutoka kwenye kaya na maeneo mengine ndani ya kijiji pamoja na kuhakikisha mpango kazi wa lishe unajumuisha  afua za chakula na lishe,afya, maji safi na usafi wa mazingira na uchangamshi kwa watoto wadogo.

 Maafisa Lishe wakimpima urefu mtoto mbele ya watendaji wa vijiji wakati wa semina ya kuwajengea uelewa maswala ya lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Desemba 18, 2023

Pamoja na kueleza wajibu wa kijiji kutokana na mkataba huo, Bi Umi aliwaeleza watendaji hao kwamba wanapaswa kushirikiana kufanya kazi kwa ufasaha ili kufikia malengo ya mkataba huo kwa kuhakikisha wanaongeza kasi kwa watoa huduma ngazi ya jamii ili kuwafikia walengwa kuongeza hamasa na ushiriki wa jamii ikiwa ni pamoja na kuongeza mwitikio na uwajibikaji wa viongozi katika usimamizi na utaratibu wa huduma za lishe kwa ngazi ya kijiji.

Afisa Lishe huyo aliwataka watendaji hao kuwaalika watoa huduma ngazi ya jamii katika mikutano ya hadhara kila mara wanapokutana na wananchi ili kuweza kuendelea kuijengea jamii uelewa wa maswala ya lishe. Pia aliwashauri watendaji hao kuielimisha jamii kuweka ziada ya chakula wakati wa mavuno na sio kuuza chakula chote ili kiisaidie jamii kwani ukosefu wa lishe bora husababisha utapiamlo ambao watu wengi katika jamii hudhani kuwa ni ushirikina.

Akiendelea kuwajengea uwezo watendaji hao, Bi Umi Kileo alisema yapo mambo ya kuzingatia katika jamii ili kuzuia utapiamlo ambapo aliwaeleza watendaji hao waendelee kuihamasisha jamii inayowazunguka kuwa na desturi  ya kula mlo kamili, kuwaelimisha  wajawazito katika maeneo yao umuhimu wa kuanza huduma ya kliniki mapema na kuwa na mahudhurio yanayoshauriwa , ikiwa ni pamoja na ushiriki wa baba  katika kuwezesha ujauzito salama na kumpunguzia mama kazi  ili kupata muda wa kupumzika kuwezesha uzazi salama “Utapiamlo hauna ushirikina ni kuzingatia Lishe bora ”, alisema Bi Umi akihitimisha mafunzo hayo kwa watendaji wa vijiji.

Watendaji wa Vijiji Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakifuatilia semina juu ya utekelezaji wa Afua za Lishe Katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ambapo walipata kujifunza mambo mengi na kuweka azimio la kuifanya ajenda ya Lishe kuwa ya kudumu kwenye vikao na mikutano ya hadhara

Msimamizi Mkuu wa shughuli za afya, Lishe na Ustawii katika Jamii Dkt Modest Buchard aliwashukuru Watendaji hao kwa kuhudhuria semina hiyo na kuwataka watendaji hao kuwa mabalozi wazuri katika jamii kwa kuifanya ajenda ya lishe kuwa ajenda ya kudumu kila wanapokuwa na vikao au mikutano ya hadhara ili jamii iendelee kuwa na uelewa mpana wa maswala ya lishe pamoja na kuzingatia vyakula venye faida katika mwili.

Mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa mitano ambayo haikufanya vizuri kwenye swala la lishe. Itakumbukwa katika ziara ya kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (MB), Desemba 16, 2023 alipotembelea Mkoa wa Geita, Mhe Mkuu wa Mkoa wa Geita ndugu Martine Shigela alimueleza Waziri kuwa hatua madhubuti zimeshachukuliwa  kwa kuweka mikakati pamoja na kuwa na nyenzo zote zinazohitajika kwenye vituo vya afya ikiwa ni pamoja na kuongeza hamasa kwa jamii kukabiliana na tatizo la Lishe Mkoani Geita.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa