• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WILAYANI GEITA WAASWA KUSIMAMIA UTAWALA BORA

Posted on: January 28th, 2025

WATENDAJI wa Kata na Vijiji wameaswa kusimamia maswala ya utawala bora katika maeneo yao ya utawala ili kuendelea kudumisha amani na utulivu.

Akizungumza na watendaji wa kata na vijiji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Januari 28, 2025 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera, Afisa TAKUKURU Mkoa wa Geita Ndg Maganga Lutunge amewataka watendaji hao kusimamia wajibu  na majukumu katika Kusimamia utawala bora ili kudumisha amani katika jamii wanazozimamia na kuziongoza na kuepusha  vurugu zinazoweza kurudisha  maendeleo nyuma.

Afisa TAKUKURU Mkoa wa Geita Ndg Maganga Lutunge akizungumza na watendaji wa kata na vijiji Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo amewataka watendaji hao kusimamia wajibu  na majukumu katika Kusimamia utawala bora

“Taasisi ya TAKUKURU imepewa mamlaka ya kudhibiti vitendo vya rushwa vinavyopelekea uvunjifu wa amani ambayo husababishwa na utawala mbovu hivyo tuzingatie utawala bora” Amesema Lutunge.

Vilevile  Ndg Lutunge  ameongeza kwa kusema vitendo vya rushwa, ubadhilifu, unyanyasaji wa wananachi, huduma duni, kutokujali wananchi, kutokuwajibika, wananchi kutokushirikishwa  katika  maamuzi yanayowahusu katika kutekeleza malengo ya serikali  na kudumisha ustawi wa wananchi yanapaswa kuepukwa kwa kuweka na kuzingatia misingi  ya utawala bora.

“Mambo mawili ya kuzingatia ili kuepuka rushwa ni kuzingatia sheria inayosimamia kazi au majukumu yenu pamoja na kuepuka kujipatia manufaa kwa kuvunja sheria kwako au kwa mtu mwingine”

Halikadhalika Watendaji wa Kata na Vijiji wamepewa elimu ya namna ya kusimamia migogoro ya ardhi katika maeneo yao ya kiutawala. Ndg, Alex Robert ni Katibu kutoka Baraza la Ardhi na nyumba Wilaya ya Geita ambapo amewataka watendaji hao  kusimamia kikamilifu  migogoro ya ardhi kupitia mabaraza ya kata katika maeneo yao ya kiutendaji. “Tuepushe malalamiko kwa kuegemea upande mmoja” Amesema Ndg Alex Robert katika mafunzo hayo.

Ndg, Alex Robert Katibu kutoka Baraza la Ardhi na nyumba Wilaya ya Geita akizungumza na watendaji wa kata na vijiji katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera ambapo amewataka watendaji hao  kusimamia kikamilifu  migogoro ya ardhi

Afisa Ardhi huyo ameongeza kwa kusema mabaraza ya kata yana mamlaka ya kupokea migogoro katika kata husika

“Mabaraza ya Kata yamepewa mamlaka ya usuluhishi tu katika migogoro ya Ardhi baada ya mabadiliko ya sheria ambapo mabaraza ya kata yanatambuliwa na sheria kuu mbili ambayo ni sheria ya mabaraza sura namba 206 toleo la mwaka 2002, sheria ya mahakama za migogoro ya ardhi sura namba 216 toleo la mwaka 2019 inayotoa mamlaka ya Mabaraza kupokea migogoro katika kata zao.  ”Amesema Ndg Alex.

Mafunzo hayo yamefanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Sheria ambayo kwa  Mkoa wa Geita ilizinduliwa na Mhe Martine  Shigela  Mkuu wa Mkoa  wa Geita  Januari 26, 2025 huku kauli mbiu ikisema “Tanzania ya 2025, Nafasi ya Taasisi zinazosimamia  Haki Madai katika Kufikia Malengo Makuu ya Dira  ya  Taifa ya Maendeleo”.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa