• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WATAKAO KIUKA TARATIBU ZA KUFANYA USAFI KUPIGWA FAINI GEITA DC

Posted on: March 1st, 2025

Katoro-Geita

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro leo 1,Machi 2025 ameshiriki katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira katika Mamlaka ya mji mdogo wa Katoro.

Akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba katika zoezi hilo la kusafisha mazingira ya Mji huo , Ndg Magaro amewataka wafanyabiasha wa Mji huo kuwa na Utamaduni wa Kufanya usafi katika maeneo yao na ambao watakiuka agizo hilo hatua kali zitachukuliwa juu yao.

" Lazima tuchukue maamuzi magumu ili Mji uwe Msafi kwa kuwapiga faini wale wote ambao watakiuka maagizo ya Serikali kwa kuwapiga faini kwa mujibu wa Sheria" Amesema Magaro.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji ndg Magaro amesema zoezi  la usafi ni endelevu na kutoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuhamasishana kufanya usafi katika maeneo yao ili kuepukana na magonjwa ya milipuko.

" Maeneo mnapofanyia shughuli zenu hakikisheni yanakuwa safi ikiwa ni pamoja na kuepuka kumwaga uchafu kwenye mitaro ya maji ili isizibe ikiwa ni pamoja na kukusanya takataka maeneo yote ya kazi ili zisisambae" Ameongeza Ndg Magaro.

Vilevile Magaro amewataka wananchi wa mji huo wa Katoro kuendelea kupanda miti  kila wanapofanya ujenzi katika makazi yao ili kuyatunza mazingira.

Kwa Upande wao Waheshimiwa Madiwani wa Kata za Katoro na Ludete ambao wameshiriki zoezi hilo wamempongeza Mkurugenzi Mtendaji  pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Geita kwa namna ambavyo wameratibu zoezi la usafi katika Mamlaka ya Mji mdogo wa Katoro.

" Nimpongeze Mhe Mkuu wa Wilaya kwa namna ambavyo ameelekeza usafi ufanyike katika mji wa katoro na Ofisi ya Mkurugenzi  kwa hamasa kubwa iliyofanywa na wananchi kujitokeza kwa Wingi" Amesema Mhe Kigongo Benedicto Diwani wa Kata ya Katoro.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Ludete  Mhe Sebastian Benedicto  amesema mji wa katoro ni mji unaokuwa kwa kasi  na kuwataka wananchi kuwa Mabalozi wa Usafi kuanzia Majumbani hadi maeneo yao ya kazi.

Zoezi la kafanya Usafi wa Mazingira ni  endelevu katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita na kila Jumamosi ya kila Mwisho wa mwezi  wananchi hujitokeza kufanya usafi kwa pamoja katika mazingira yao katika kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, la kuhakikisha mazingira yana kuwa safi na Salama.

Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • GEITA DC KUENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA BOOST YENYE THAMANI YA BILIONI 3.2

    October 09, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NYANG'WALE ATEMBELEA BANDA LA MAONESHO YA MADINI LA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

    September 24, 2025
  • WAUGUZI WA AFYA NA MAAFISA LISHE GEITA DC WAASWA KUEPUKA MIGOGORO MAENEO YA KAZI.

    September 22, 2025
  • WANANCHI KATORO WAJITOKEZA KUADJIMISHA SIKU YA USAFISHAJI DUNIANI.

    September 20, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa