• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WARATIBU LISHE WAHIMIZWA ELIMU KWA AKINA MAMA WAJAWAZITO, GEITA DC.

Posted on: August 20th, 2024

Agosti 20,

WARATIBU lishe nchini wamesisitizwa kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha kwa akina mama wajawazito ili kuwasaidia kujifungua salama, pamoja na kupunguza madhara ambayo yanaweza kuwakumba watoto wachanga baada ya kuzaliwa.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyoendeshwa kwa siku mbili kwa Waratibu wa Lishe wa vituo vya kutolea huduma za afya, yakijumuisha vituo 13 vya Wilaya ya Geita vijijini, Afisa Lishe wa Mkoa, Bi Naomi Andrea Rumenyela amewataka wahudumu hao kuweka mkazo wa lishe bora kwa akina mama wajawazito pamoja na kuhakikisha wanatembelea vituo vya afya mara kwa mara pindi wanapojigundua kuwa ni wajawazito.

Aidha Bi Naomi pia amewataka wahudumu wa afya kuhakikisha wanajaza kwa usahihi taarifa za  akina mama wajawazito, (Maoteo) kwenye vituo vyao ili dawa zinazotolewa  kwa  wajawazito ziweze kukidhi haja ya wajawazito ikiwa ni pamoja na kupunguza idadi ya kina mama wanaopatwa na tatizo la ukosefu wa damu ya kutosha pindi wanapojifungua.

"Hakikisheni wakati wa kujaza taarifa za akina mama wajawazito, mnaweka taarifa sahihi kwenye mfumo ili Bohari ya Dawa ya Taifa (MSD) wanapotoa dawa, ziweze kuwafikia kama mlivyoagiza ili kupunguza tatizo la wajawazito wanaopoteza maisha kutokana na upungufu wa damu."Amesema Bi Naomi.

Afisa Lishe wa Mkoa, Bi Naomi Andrea Rumenyela akiwaelezea Waratibu Lishe kutoka Wilaya ya Geita kuhusiana na lishe bora kwa akina mama wajawazito ili kuepukana na changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa kujifungua.

Pamoja na hayo, Bi Naomi pia amewataka waratibu hao wa lishe wahakikishe wanawahimiza akina mama waonyonyesha kuwapatia watoto wao maziwa ya mama, ambayo yana protini yakutosha, ikilinganishwa na maziwa mbadala ya ng’ombe.

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Nasim Ginga amesema kuwa, wahudumu wa afya wanapaswa kuandika dawa zinazotumiwa na wajawazito, pamoja na  kujaza kwa usahihi kitabu cha afya ya mtoto, kwa kuzingatia urefu, uzito na umri wa mtoto husika, ili taarifa zinazoletwa kutoka vituoni ziwe sahihi.

Vilevile Bi Nasim amewashauri Waratibu Lishe kuhusiana na kufanya tathmini ya kina ya hali ya lishe na ulaji wa mama wajawazito kabla, na baada ya kujifungua. "Ni muhimu kwa sisi kama wahudumu wa afya kupata taarifa za mlengwa kuhusu chakula anachotumia, mwenendo wa ulaji, na ni  wakati gani hua anakula. Hii itasaidia kutokomeza changamoto ya utapiamlo miongoni mwa wajawazito, pamoja na watoto." Amesema Bi Nasim.

Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Nasim Ginga akitoa ufafanuzi kuhusu umuhimu wa Waratibu Lishe kuhakikisha wanajaza taarifa kwa usahihi za mama na mtoto wakiwa vituoni.

Kwa upande mwingine Mratibu wa Lishe kutoka kituo cha afya Nzera, Bwana Charles Kafulela amesema kuwa, kama wahudumu wa afya, wameweza kupata elimu ya kutosha kuhusu afya ya mama na mtoto ambayo itasaidia kukabiliana na changamoto za kiafya zinazoweza kujitokeza pindi mama akikosa lishe bora.

"Mafunzo yapo vizuri na tumeweza kupata vitu vingi ambayo tutavihitaji tukiwa kazini, pamoja na kujifunza vitu gani mama anapaswa kufanya ili kuwa na damu ya kutosha, pamoja na kuwa na afya bora yeye na mtoto ajaye."Amesema Bw Kafulela.


Baadhi ya Waratibu Lishe kutoka vituo vya afya tofauti Wilayani Geita waliojitokeza kwenye mafunzo yaliyolenga kuwapatia ujuzi zaidi kuhusiana na kutatua changamoto zinaweza kujitokeza kwa wazazi na watoto kutokana na lishe isiyo bora.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa