• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAOMBA UWEPO WA ASKARI WA USALAMA BARABARANI KITUO CHA MABASI IHUMILO KATA YA NKOME WILAYANI GEITA

Posted on: November 8th, 2023

Na Hendrick Msangi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Ihumilo kata ya Nkome Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu  Tumaini Christopher ameiomba Serikali kupeleka askari wa usalama  barabarani kwenye kituo cha mabasi Ihumilo ambacho hakifanyi kazi kwa sasa Licha ya kuwa na miundombinu yote inayohitajika katika kituo hicho.


Hayo yameelezwa Novemba 7, 2023 wakati timu ya utawala (CMT) ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ikiongozwa na Mkurugenzi wake Ndugu Karia Rajabu Magaro ilipotembelea kituo hicho cha mabasi kwenye kata hiyo ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa kutembelea miradi inayoendelea kwenye Halmashauri hiyo.

Timu ya utawala (CMT) ikiongozwa na Mkurugenzi wake Ndugu Karia Rajabu Magaro walipotembelea kituo cha mabasi Ihumilo kata ya Nkome.


Kituo hicho cha mabasi kilianza kutumika Januari 03, 2020 lakini baadaye kilisimama kufanya kazi kwani magari licha ya kuwa na jengo la kupumzika abiria, huduma za choo, kituo kidogo cha kukaa askari polisi lakini magari hayafi kituoni jambo ambalo linafanya mradi huo kuharibiwa miundombinu yake. 

" Tunamuomba Mhe Diwani kutoa ushirikiano wa kutosha katika kufanya hamasa ya kuendeleza kituo ili magari yaweze kufika na ushuru ukusanywe eneo la kituo cha mabasi kwani kwa sasa anayekusanya ushuru analazimika kuyafuata magari sehemu ambayo sio kituo sahihi" alisema Mwenyekiti Huyo.


Akiongoza timu hiyo Mkurugenzi Magaro aliwataka Viongozi hao wa serikali ya kijiji na kata kuchukua hatua madhubuti ili kituo hicho cha mabasi kiendelee kufanya kazi kama ilivyo kuwa awali. 

" Fanyeni usafi wa kituo hiki kuyatunza mazingira na miundombinu yake ambayo inaharibiwa kutokana na kituo cha mabasi kutokufanya kazi, " alisema Magaro.


Pamoja na ziara katika kituo hicho cha mabasi, timu hiyo iliweza kutembelea mradi wa kituo cha afya Nkome wenye jengo la OPD, maabara na jengo la Upasuaji ambapo fedha za mradi huo ni jumla ya kiasi cha shilingi milioni miatano ( 500,000,000) kutoka CSR.

Mradi wa Kituo cha afya kata ya Nkome unaotekelezwa kwa fedha za CSR kiasi cha shilingi 500,000,000.

Mkurugenzi aliwataka wakandarasi wanaotekeleza mradi huo kuongeza kasi kwa kuwa fedha za mradi zipo.

 "Kazi zifanyike kwa wakati kwani Serikali imekwisha tenga fedha za mradi zipo hakuna sababu ya kuchelewesha ukamilishwaji wa mradi huu" alisema Magaro.

CMT wakikagua mradi wa wa kituo cha afya Nkome. Mkurugenzi alitoa maagizo kwa Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kuongeza kasi na kuhakikisha kuna Kuwa na mafundi wa kutosha ili kazi ifanyike kwa uharaka.

Mradi huo kwa mujibu wa mkataba wake unatarajiwa kukamilika Desemba 30,2023 ili wananchi waweze kupata huduma.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuipatia fedha nyingi kukamilisha miradi mbalimbali na kuleta maendeleo kwa Watanzania.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa