• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WAASWA KUYATUNZA MAZINGIRA NA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Posted on: November 26th, 2024

Wanafunzi waliomaliza mitihani ya kidato cha nne 2024 katika shule ya Sekondari Bugalama Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Novemba 26, 2024 wamejumuika pamoja na walimu na viongozi wa chama na serikali  katika zoezi la upandaji wa miti na uchangiaji wa damu salama.

Awali akizungumza katika zoezi hilo Mkuu wa shule ya Sekondari Bugalama Mwl Gibson Petro Mkomi amesema shule hiyo  yenye jumla ya wanafunzi 616 inazingatia misingi ya utoaji elimu bora, nidhamu kwa walimu na wanafunzi  na utunzaji wa mazingira.

“Wanafunzi  wetu waliomaliza kidato cha nne mwaka huu 2024 wameona  watoe zawadi ya upandaji wa miti katika kutunza mazingira na kuchangia  utoaji wa damu salama ili kusaidia jamii ambayo inapitia changamoto za upatikanaji wa damu.

Wanafunzi wakisikiliza elimu juu ya uchangiaji wa damu, kutoka kwa Afisa Mteknolojia maabara kitengo cha Damu salama Hospitali ya wilaya - Nzera

Aidha Mwalimu Mkomi amesema shule hiyo inazingatia utunzaji wa mazingira ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika upandaji  wa miti ili kutunza mazingira .

“Tumeandaa miti 500 ambayo kati ya hiyo miti 100 ni miti ya matunda, 100 miti ya kivuli na miti 300 ya mbao ambayo imekuwa ikisaidia kutengeneza samani za shule pamoja na kuongeza pato la shule kipindi inapovunwa.” Ameongeza Mwl Mkomi.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Bugalama, Mwl Gibson Mkomi akiongoza zoezi la upandaji miti katika shule ya Bugalama

Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalum Mhe Veronica Migelegele amewataka wanafunzi na walimu kuitunza miti waliyoipanda ili kuendelea kuunga juhudi za Mhe Rais za utunzaji wa Mazingira na kuwataka kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024”

“Tuyatunze mazingira na tushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili tupate viongozi bora kwa ajili ya kuongoza katika maeneo yetu na kuchochea maendeleo.” Amesema Mhe Migelegele

Diwani wa Viti Maalum Mhe Veronica Migelegele akizungumza mbele ya wananchi na wanafunzi waliojitokeza katika zoezi la upandaji wa miti na uchangiaji wa damu salama.

Wanafunzi hao wameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwaboreshea mazingira mazuri ya kujifunzia ndio maana wameweza kurudi shuleni licha la kumaliza mitihani ili kuungana na wanafunzi wenzao wa vidato vya chini katika kupanda miti na kuchangia damu.”Tumepanda miti ili kuendelea kuboresha mazingira mazuri ya  shule yetu pamoja na kuzuia mmomonyoko wa udongo ambao unaweza kuleta athari katika maeneo yetu. Amesema Dionizi Katisho mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne.

Pamoja na zoezi hilo  wanafunzi hao, walimu pamoja na viongozi wa chama na serikali walioshiriki katika upandaji wa miti, wamechangia  utoaji wa damu salama lililoratibiwa na watoa huduma kutoka Hospitali ya Wilaya iliyopo Nzera.

Zoezi la upandaji wa miti likiendelea katika shule ya sekondari Bugalama

Akizungumzia umuhimu wa kuchangia damu, Afisa Mteknolojia Maabara kitengo cha damu salama kutoka Hospitali ya Wilaya ya Geita-Nzera, Bi Petty Mzumbwe amesema upo umuhimu wa jamii kuchangia damu kwa kuwa hakuna kiwanda cha kuzalisha damu kuwasaidia wagonjwa wenye uhitaji katika maeneo mbalimbali nchini.


zoezi la uchangiaji wa Damu salama.

Shule ya Sekondari Bugalama  ilianza mwaka 2009 na imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani ya kitaifa ambapo kwa mwaka 2023 iliweza kuwa ya kwanza na kuongoza kati ya shule 44 za Serikali kwa matokeo mazuri katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa