• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI KISIWA CHA IZUMACHELI WAPEWA ELIMU AFUA ZA LISHE

Posted on: January 30th, 2025

LISHE ni jambo ambalo Limepewa kipaumbele kikubwa na Serikali ya awamu ya Sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika kuunga Juhudi za Serikali kutekeleza afua za Lishe, Januari 30,2025 maafisa Lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita wametembelea Kisiwa cha Izumacheli kilichopo ziwa Viktoria kwa ajili ya kutoa elimu  ya Lishe kwa wananchi kisiwani humo.

Akizungumza katika Mafunzo hayo Afisa Lishe Bi Nasim Ginga amesema lengo kuu la wao kutembelea kisiwani Izumacheli ni kutoa elimu  ya namna ya kuandaa chakula bora  kilichozingatia makundi yote ya chakula pamoja na kutathimini hali ya Lishe ipoje  ukanda wa Kisiwa cha Izumacheli.

Wananchi hao wameelekezwa kuandaa uji wa Lishe kwa kuzingatia upatikanaji wa vyakula vinavyopatikana katika mazingira yao.

Kwa upande wake Mapembe Gamva ambaye ni mkazi wa Izumacheli amesema Elimu hiyo ni muhimu sana kwao katika kusaidia watoto kupata Lishe bora kwa ajili ya ustawi wa afya zao.

Halikadhika Ndg Chuga Nistasi amesema ataitumia elimu hiyo kumuelekeza mke wake namna ya kuandaa Uji wa Lishe kwa kuzingatia upatikanaji wa vyakula vinavyopatikana katika Kisiwa hicho.

Naye Bi Zena Lawson (27) mkazi wa Kata ya Izumacheli ni mwanamke mwenye watoto  wa tano ambapo ameishukuru Serikali kwa namna ambavyo inawajali wananchi waishio visiwani kwa kuwapatia elimu ya maswala ya Lishe.

Akihitimisha zoezi la utoaji wa elimu ya Afua za Lishe, Bi Ummy Kileo, Afisa Lishe Halmashauri ya Wilaya ya Geita amesema zoezi hilo  litaendelea kufanyika mara kwa mara katika Kisiwa hicho.

Makundi  ya Vyakula ambavyo wananchi wameshauriwa kula ni pamoja na vyakula vya nafaka, mizizi  na ndizi za kupika, Vyakula vya asili ya wanyama, vyakula vya jamii ya mikunde, mbogamboga, Matunda, mafuta na maji ambayo sio kundi  la chakula  lakini ni muhimu sana kwa afya.

Wananchi Kisiwani Izumacheli wakielekezwa namna ya kuandaa uji wa lishe kwa kutumia mahitaji yanayopatikana katika mazingira yao


Afisa Lishe Bi Ummy Kileo akimuhudumia Mwananchi katika Kisiwa cha Izumacheli walipotembelea kutoa elimu ya afua za Lishe katika kata hiyo iliyopo kisiwani


Maafisa Lishe Kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita Wakiwahudumia Wananchi wa Kata ya Izumacheli walipowatembelea kutoa mafunzo ya Afua za Lishe


Mtendaji wa Kata ya Izumacheli, Alfred Conrad akiwamiminia uji wa lishe wananchi waliojitokeza katika mafunzo hayo

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa