• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI KATA YA IZUMACHERI KUONGEZEWA KIVUKO KURAHISISHA SHUGHULI ZA MAENDELEO.

Posted on: March 12th, 2024

Na: Hendrick Msangi

Wananchi wa kisiwa na kata ya Izumacheli Wilayani Geita, wamekumbwa na changamoto ya kushindwa kupeleka mazao ya samaki pamoja na biashara zingine kutokana na kivuko cha MV Tegemeo kuwa na safari moja hivyo kupelekea adha na shida ya usafiri katika maeneo yao.

Baadhi ya wananchi wa eneo hilo wameeleza kuwa, pamoja na uwepo wa kivuko hicho lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya usafiri kutokana na kwamba usafiri huo umekuwa ukisafirisha abiria mara moja kwa siku na kupelekea kusimama kwa baadhi ya shughuli.

Aidha, wananchi hao wameeleza kuwepo kwa changamoto ya mawasiliano hususani katika miundombinu ya usafiri na ucheleweshwaji, hivyo wanahitaji vivuko na usafiri wa njia ya maji ili kurahisisha shughuli mbalimbali na kufika katika maeneo mengine kwa wakati, Kutokana na  jiografia ya eneo hilo pia wameomba kuwepo kwa vivuko vya kujitosheleza kutokana na mahitaji yao

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Mhe Fadhili Maganya amewataka watumishi na viongozi wilayani Geita kutoka kwenye ofisi zao na kwenda kuwasikiliza wananchi ili kutatua kero zao badala ya kusubiri  viongozi wa kitaifa kufika.

Akizungumza katika Mkutano wa hadhara kufuatia ziara hiyo ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa,Diwani wa kata ya Izumacheli, Mhe Cosmas Fideli amekiri kuwepo kwa changamoto ya usafiri wa kivuko hicho, na kueleza kutokana na shida hiyo wananchi wanakosa huduma kwa wakati na kupelekea shughuli za uchumi kusimama kutokana na kushindwa kupeleka bidhaa sokoni kwa  muda unaohitajika kutokana na kivuko hicho kufanya safari zake  mara moja kwa siku. Pia ameongeza kuwa kuna baadhi ya vijiji havina kivuko na inawabidi kutumia mitumbwi midogo ambayo inahatarisha usalama wa wananchi.

Kufuatia kilio hicho Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita, Barnabas Mapande amemuomba Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Mhe Fadhili Maganya kuwasaidia kufikisha kilio hicho cha wananchi ili kiweze kutatuliwa kutokana na shida ya kivuko inayowakabili, na kuiomba TEMESA iweze kuwasaidia kutatua changamoto hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Msukuma ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuletea fedha nyingi za miradi katika Wilaya ya Geita ikiwepo ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami umbali wa kilometa 20 kutokea kutokea Kata ya Nkome hadi kijiji cha Sungusira kata ya Nzera.

Aidha, Mbunge wa jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Msukuma ameahidi kulishughulika tatizo hilo, na kueleza  kuwa Serikali imelipokea na inalifanyia kazi suala hilo, na kusema daraja la Busisi litakapokamilika vile vivuko vitapelekwa katika kisiwa hicho ili kukidhi mahitaji ya wananchi hao, na kuwahakikishia wananchi wa kisiwa hicho kuwepo kwa safari mbili hadi tatu kwa siku ili kutatua changamoto ya wananchi ya kukosekana kwa kivuko kwa wakati kwasababu kivuko kilichopo kinapita mara moja tu kwa siku.

Akiendelea na ziara hiyo Mwenyekiti huyo wa Jumuiya ya Wazazi Taifa aliitembelea kata ya Nkome ambayo wakazi wake wengi hujishughulisha na uvuvi ambapo alisikiliza kero za wananchi na kuwataka watumishi kuwatembelea wananchi ili kusikiliza kero zao ili kuepuka kusubiri viongozi wa kitaifa kufika katika maeneo ya wananchi kwani zipo kero ambazo zinaweza kumalizwa pasipo viongozi wa kitaifa kufika.

Wananchi wa Kata ya Nkome wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Mhe Fadhili Maganya ambapo walieleza kero zao na kupatiwa ufumbuzi

Pamoja na hayo aliigaza ofisi ya Mkuregenzi Mtendaji kufuatilia swala la ardhi kwa ajili ya upatikanaji wa eneo la kujenga mradi mkubwa wa soko la samaki pamoja na uwepo wa askari polisi wa kike katika kituo cha polisi kwenye kata ya Nkome.

Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Wilayani Geita na Watumishi wa Halmashauri wakiwa kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mhe Fadhili Maganya alipofanya ziara Wilayani Geita katika kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Wakati huo huo Mbunge wa jimbo la Geita Vijijini Mhe Joseph Msukuma aliishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipendelea Geita kwa kutoa fedha nyingi za miradi ukiwepo mradi wa kituo cha Afya Nkome ambao utakapokamilika wananchi wa kata hiyo watanufaika na huduma za afya ikiwa ni pamoja na urefu wa barabara kwa kiwango cha lami kilometa 20 kutokea Kata ya Nkome hadi kijiji cha Sungusira kata ya Nzera.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa