• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MAMA SAMIA LEGAL AID COMPAIGN (MSLAC) YALETA MATUMAINI MAPYA KWA WANAFUNZI GEITA DC

Posted on: January 29th, 2025

Timu ya Msaada wa Kisheria ijulikanayo kama Mama Samia Legal Aid Compaign (MSLAC ) imeendelea na Kampeni ya utoaji wa elimu ya msaada wa kisheria katika Kata ya Magenge Halmashauri ya Wilaya ya Geita Januari 29,2025.

Timu  hiyo imetembelea Shule ya Sekondari Magenge  yenye Jumla ya wanafunzi 450 wanaume wakiwa  264 na Wasichana 186 na shule ya Msingi Magenge yenye Jumla ya wanafunzi 904 Wavulana wakiwa 465 na Wasichana 439.

Wanafunzi hao wamepewa elimu  juu ya Ukatili  wa Kijinsia na Haki za Watoto na wametakiwa kutoa taarifa  za unyanyasaji pale wanapo ona viashiria vya unyanyasaji. 

"Kesi za Ukatili zimepewa kipaumbele na zinashughulikiwa zikiwepo kesi za  ubakaji, hivyo mtoe taarifa mapema pindi  mnapopitia hali yoyote ya ukatili katika maeneo yenu"  Amesema Koplo Salome kutoka dawati la Jinsia Geita.

Aidha WP Salome amewaasa wanafunzi hao kuepukana na  tabia za mahusiano ya kimapenzi wawapo shuleni  kwani tabia hizo zinakatisha ndoto zao.

Akizungumza kuhusu haki  za watoto Mhe Doreen ambaye ni Wakili kutoka Chama cha Mawakili Tanzania (TLS) amewakumbusha wanafunzi hao juu ya haki  zao ikiwa ni pamoja na haki ya kulindwa.

" Serikali imewekeza miundombinu ya kuwalinda ili msiharibikiwe" Amesema Wakili Doreen.

Aidha wakili huyo amewataka watoto hao kuziishi ndoto zao na kuepuka watu ambao wanakatisha ndoto zao na kuwataka kujilinda kuanzia  nyumbani. 

"Anzeni kujisimamia kuanzia sasa ili mfikie malengo yenu kwa kuepuka kujihusisha na kazi ambazo zinahatarisha maisha yenu. Muwe na uhuru wa kutoa taarifa mapema ili kujisaidia" Ameongeza Wakili.

Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya Sekondari Magenge wameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutambua changamoto  wanazopitia na kuwaletea huduma ya msaada wa kisheria. 

Ngasani Forodhani na Edwin Evaristi  ni wanafunzi wa kidato cha nne katika shule hiyo, wameeleza ukatili uliopo majumbani  unaotokea kati ya wazazi na kutaka kujua sehemu ya kupata msaada huku wakionyesha hali ya wasiwasi  iwapo wazazi watapelekwa jela pindi  wanapotoa taarifa za ukatili unaotokea majumbani.

" Mzazi ikitokea akifungwa itakuwa kama  laana kwetu kwa kuwa tumetoa taarifa na jambo hili linatufanya kuwa na wasiwasi na kusababisha kuwa na uoga kutoa taarifa za ukatili." Amesema Ngasani

" Ninayo furaha kwa sababu  Serikali inatukumbuka sisi wanafunzi ila wazazi  wamekuwa sehemu ya kukwamisha ndoto zetu na tunakuwa na wasiwasi kutoa taarifa kwa walimu juu ya wazazi wanao tufanyia vitendo vya ukatili " Amezungumza kwa hisia Erick Evaristi mwanafunzi wa kidato cha nne. 

Akiwatoa wasiwasi wanafunzi  hao, WP Salome ametaka wanafunzi hao kutoa taarifa kwa watu wanao waamini huku akitoa wito kwa walimu kuwasaidia wanafunzi juu ya changamoto wanazopitia.

Naye  Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Magenge Mwl.George Mgaya  ameishukuru Timu hiyo kwa kutembelea shule ya Magenge  kutoa elimu ya Ukatili wa Kijinsia na Haki za Watoto na kusema shule hiyo ni miongoni mwa shule sita zinazotekeleza mpango wa Elimu salama Mkoani Geita.

Zoezi la utoaji wa elimu juu ya msaada wa kisheria kwa wananchi linaendelea  na jumla ya kata 10 zinatarajiwa kufikiwa na Timu hiyo ya Mama Samia Legal Aid Compaign (MSLAC )

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa