• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI YA SERIKALI KWA UADILIFU.

Posted on: November 30th, 2024

Viongozi wateule wa Serikali za Mitaa Wilayani Geita, wametakiwa kuweka mbele maslahi ya Kitaifa kwa kuhakikisha waisimamia kwa uweledi na uaminifu miradi ambayo inatekelezwa na Serikali pamoja na kuwatumikia wananchi bila kujali tofauti zao za kisiasa.

Akizungumza hapo jana kwenye hafla ya Uapisho wa viongozi wa nyanja tofauti za Serikali za Mitaa wakiwamo Wenyekiti wa Mitaa, Vitongoji, Vijiji, pamoja na Wajumbe kutoka Kata za Katoro, Nyamigota, Ludete, Kaseme, pamoja na Magenge, katika ofisi za Kata, Katoro pamoja na Shule ya Sekondari Magenge Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Halmashauri ya Wilaya Geita, Bw. Abdallah Mkumbo, amesema kuwa Uongozi ni dhamana na hivyo viongozi ngazi ya kata wanapaswa kuwajibika na kufanya kazi kwa kusimamia kikamilifu miradi inayotekelezwa na serikali, kwa manufaa ya wananchi, na taifa kwa ujumla.


“Mnapaswa kufahamu kuwa nafasi mlizozipata ni dhamana kutoka kwa wananchi ambao wamewaamini na hivyo mnapaswa kuwatumikia kwa uweledi bila kujali itikadi zao. Miradi inaendelea kutekelezwa kwahiyo mnapaswa kuisimamia kwa uadilifu mkubwa ili iweze kuwa na tija kwa wananchi.” Amesema Bw. Mkumbo.

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Wilaya, Bw. Abdallah Mkumbo amewataka Wenyekiti wa Mitaa, Vitongoji, Vijiji, pamoja na Wajumbe kuhakikisha wanasimamia miradi inayotekelezwa na serikali kwa uadilifu na maslahi ya taifa kwa ujumla.


Kwa upande mwingine, Hakimu Mkazi kutoka Mahakama ya Mwanzo Katoro, Wakili Adam W. Mashiba, amewataka viongozi hao kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, na taratibu na kuyaishi yale waliyoyatamka kwenye viapo vyao.


“Hakikisheni mnafanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, na taratibu zilizowekwa katika utumishi wenu kwa wananchi. Viapo vyenu vina maana kubwa na hivyo mnatakiwa mvitekeleze kwa vitendo mkizingatia Utii, Uadilifu na kutunza siri.” Amesema Wakili Mashiba.

Hakimu Mkazi kutoka Mahakama ya Mwanzo Katoro, Wakili Adam W. Mashiba akitoa maelekezo kwa Wenyetiki wateule wa Mitaa kutoka Kata za Katoro, Nyamigota, Ludete, Kaseme, na Magenge ya namna ya ujazaji wa fomu za viapo.


Aidha, kwa upande wa viongozi, Bw. Mussa William Kaniki aliyeshinda kiti cha Uwenyekiti wa Kilimahewa, Kata ya Ludete kwa tiketi ya CCM amesema kuwa atahakikisha anawahudumia wananchi na kuwatetea kwa usawa pasi na kujali tofauti zao za kisiasa, huku akitoa pongezi kwa namna zoezi zima la uchaguzi lilivyoendeshwa.

Baadhi ya Wenyekiti wa Mitaa, Vitongoji, Vijiji, pamoja na Wajumbe kutoka Kata za Katoro, Nyamigota, Ludete, Kaseme, na Magenge wakila kiapo cha Uaminifu, Utii, pamoja na Kutunza siri, mbele ya Hakimu Mkazi kutoka Mahakama ya Mwanzo Katoro, Wakili Adam W. Mashiba katika ofisi za Kata, Katoro na Shule ya Sekondari Magenge.

Zaidi ya viongozi 100 kutoka kata za Katoro, Nyamigota, Ludete, Kaseme, na Magenge walikula kiapo hapo jana kutokana na uchaguzi wa Serikaliza Mitaa uliofanyika mnamo tarehe 27, Novemba, 2024.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa