• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WA UMMA WAASWA KUWA WAADILIFU KATIKA UTUMISHI WAO

Posted on: March 6th, 2025

Geita

VIONGOZI wa umma Mkoani Geita wametakiwa kuwa waadilifu katika Utumishi wao ili kuendelea kuweka imani kwa wananchi  katika maeneo yao ya kiutawala.

Hayo yameelezwa leo Machi 6,2025 katika Kikao Kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela akifungua mafunzo ya Maadili kwa Viongozi na Watumishi wa Umma Katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita 

Awali akifungua mafunzo hayo yaliyoendeshwa na Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela ameipongeza  Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kuendelea kufanya maboresho ya mifumo  ambayo inapelekea kuwa na wepesi kwa viongozi wa umma katika utendaji na utoaji wa taarifa.

Aidha Mhe Shigela ametoa pongezi na kuwashukuru Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Geita kwa utendaji kazi wao uliopelekea kupunguza malalamiko kwa wananchi katika maeneo yao huku akiwasihi viongozi hao kuzingatia mafunzo hayo muhimu.

Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi na Watumishi wa umma Kanda ya Ziwa Ndg Godson Kweka akizungumza katika Mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa umma Mkoani Geita 

Akizungumza katika Mafunzo hayo Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi na Watumishi wa umma Kanda ya Ziwa Ndg Godson Kweka amesema lengo la Mafunzo hayo ni kuendelea kuwakumbusha viongozi mambo ya Msingi ya Maadili ambayo wanatakiwa kuyatekeleza kwa kuzingatia sheria za Maadili.

Mwezeshaji Kutoka Ofisi ya Maadili,  Kanda ya Ziwa Wakili Msomi Abigael Majige akitoa mada ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika Mafunzo yaliyofanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

Kwa upande wake Mwezeshaji Kutoka Ofisi ya Maadili,  Kanda ya Ziwa Wakili Msomi Abigael Majige amewataka viongozi hao kuzingatia Uadilifu katika Utendaji wao kwa kuwa ndio nguzo katika kuwaletea wananchi Maendeleo.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro(Kulia aliyevaa miwani) akifuatilia mada Katika Mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa umma katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita 

"Maamuzi mnayoyafanya yana athari kubwa kwa wananchi hivyo tuzingatie maadili katika kufanya maamuzi kwa kuzingatia ukweli na uadilifu" Amesema Majige.

Pamoja na hayo Wakili Majige amewakumbusha viongozi hao kuwa wa wazi katika kutoa tamko la Rasilimali na madeni.

Vilevile wametakiwa kuwa na mwenendo mzuri wenye tabia nzuri  kwa kuepuka matumizi mabaya ya madaraka.

" Tutumie dhamana tulizopewa tukijua vyeo tulivyo navyo ni dhamana ili tuweze kuwahudumia wananchi waweze kuwa  na imani na Serikali yao" Ameongeza Wakili Majige.

Halikadhalika Viongozi wa Umma wametakiwa kufanya maamuzi kwa kuzingatia misingi ya sheria,  kanuni na taratibu pasipo upendeleo katika kutoa huduma kwa kuwa na lugha nzuri kwa wananchi kuondoa mgongano wa maslahi.

Viongozi mbalimbali wa Umma Mkoani Geita wakiwa Katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita katika Mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa umma 

Mafunzo hayo wamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwepo Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa Geita,  Wakuu wa Wilaya,  Makatibu Tawala Wilaya,  Viongozi wa Ulinzi na Usalama na Wakuu wa Idara na Vitengo katika Halmashauri za Mkoa wa Geita.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa