• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA GEITA DC WAPATIWA MAFUNZO YA UTAWALA BORA NA ELIMU YA URAIA

Posted on: February 4th, 2025

Nzera-Geita

VIONGOZI wa Serikali za Mitaa na Watumishi Viongozi Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Februari 4,2025 wamepewa mafunzo ya Uraia na utawala bora ili kuwajengea  uelewa mpana katika Utekelezaji wa Majukumu yao.

Awali akifungua Mafunzo hayo kwa Niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba,  Katibu Tawala wilaya ya Geita Bi Lucy Beda amewataka viongozi hao kupeleka maarifa na ujuzi kuanzia  ngazi ya familia na maeneo ya kazi.

Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda akizungumza katika Mafunzo ya Elimu ya uraia na utawala bora katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera 

"Ninafahamu kuwa wote mnaoshiriki mafunzo haya mnawakilisha kundi kubwa la watumishi walio chini yenu, hivyo Niwaombe msiwe wachoyo, pelekeni elimu mtakayoipata katika mafunzo haya kwa watumishi wengine" Amesema Bi Lucy Beda.

Aidha Katibu Tawala huyo ameongeza kwa kusema mafunzo hayo yamefanyika  wakati muafaka kwa kuwa Wilaya ya Geita kumekuwepo changamoto katika Utekelezaji wa haki za Binadamu.

Pamoja na hayo Bi Lucy Beda ametoa rai kwa viongozi hao kwenda kuyatumia mafunzo waliyopatiwa kama chachu ya kuleta mabadiliko katika usimamizi ulinzi wa haki za Binadamu na misingi ya utawala bora ili kukuza Demokrasia na kudumisha amani na utulivu katika Wilaya ya Geita na Nchi  kwa ujumla wake.

Akizungumza katika Mafunzo hayo Mratibu wa Mafunzo Mhe Joyce Mushi ambaye ni Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria amesema Wizara ya Katiba na Sheria imeendelea kuwezesha utatuzi wa Migogoro mbalimbali kwa kuendelea kutoa elimu ya masuala ya uraia na utawala bora kwa viongozi na watendaji wa Serikali za Mitaa.

" Wizara ya Katiba na Sheria ni moja  ya vinara wa utekelezaji wa 4Rs ambazo ni Maridhiano( Reconciliation) Ustahimilivu ( Resilience) Mabadiliko ( Reforms) na Kujenga upya (Reconstruction)" Amesema Mhe Joyce Mushi.

Aidha Wakili Mushi  amesema lengo la Wizara ya Katiba na Sheria kutoa mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo viongozi ili waweze kutekeleza majukumu yao pasipo kuvunja sheria, vilevile kuendelea kuwajengea viongozi uwezo wa masuala ya haki na wajibu, demokrasia na utawala bora, madaraka ya umma na ulinzi na usalama.

Vilevile Wakili huyo ameongeza kwa kusema kupitia mafunzo hayo viongozi wataendelea kupata uelewa kukuza na kuendeleza uzalendo na utaifa, na kuweza kujua namna ambavyo wanaweza kushughulikia malalamiko ya wananchi katika ngazi zao za utawala kwa ufanisi na ueledi.

Pamoja na hayo  Wakili Mushi  amewataka Viongozi hao kupitia elimu waliyopata kuifikisha katika ngazi au viongozi walio chini yao wakiwemo wenyeviti wa Vijiji,  Mitaa na Vitongoji.

Halikadhika Viongozi hao  wametakiwa kwenda kutekeleza majukumu yao kwa kujiamini kwa kufuata Misingi ya Demokrasia na Utawala bora.

Mafunzo hayo ya elimu ya uraia na utawala bora yametolea katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera ambapo mada mbalimbali zimewezeshwa katika mafunzo hayo ikiwemo mada ya Demokrasia na Utawala bora,  Haki na Wajibu,  Ulinzi na Usalama  pamoja na Madaraka kwa umma.

Watendaji wa kata Wakiwa katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera ambapo wamejifunza elimu ya uraia na utawala bora

Mafunzo hayo yametolewa na Wataalam kutoka Wizara ya  Katiba na Sheria,  Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora na Jeshi la  Polisi ambapo  walengwa katika mafunzo hayo walikuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama,  baadhi ya wakuu  wa divisheni za Halmashauri na watendaji wa kata.

Mafunzo ya Elimu ya uraia na utawala bora yamekwishatolewa katika Mikoa mitano kwa awamu ya kwanza na sasa ni awamu ya pili inaendelea kutolewa katika mikoa 6 hivyo kupelekea jumla ya mikoa 11 ambayo ni Rukwa, Mara, Songwe, Uringa, Morogoro, Kigoma,Geita Katavi,Katavi, Tabora,  Mtwara na Kilimanjaro

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa