Huku Serikali ikiwa inaendelea na juhudi za kuhakikisha huduma za kijamii zinawafikia wananchi haswa maeneo ya vijijini, kamati mbali mbali ambazo zimeundwa kusimamia utekelezaji wa miradi hio, hususani kwenye nyanja za Elimu na Afya, zimetakiwa kuhakikisha zinafuafilia hatua kwa hatua ukamilishaji wa miradi hiyo ili wananchi waweze kupata huduma kwa haraka.
Akizungumza tarehe 11, Juni kwenye mwendelezo wa ziara maalumu ya ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Wilaya ya Geita katika Tarafa ya Busanda, Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu, Bi. Sarah Yohana, kwa niaba ya Mkurugenzi, amewataka wenye dhamana ya usimamizi wa miradi hiyo, kujikita kwenye maeneo ya muhimu kwa miradi iliyopo katika hatua za ukamilishaji.
Bi. Sarah ameongeza pia kwa kusema, Watendaji wa Kata wana wajibu wa kuhakikisha kuwa wanaitambua miradi iliyopo kwenye maeneo yao, pamoja na kufuatilia fedha ambazo zimetengwa na Halmashauri kwaajili ya kumalizia miradi hiyo.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa