• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

TUKAWATUMIKIE WANANCHI KATIKA NAFASI ZETU KUCHOCHEA MAENDELEO-MSIMAMIZI MSAIDIZI BI SARAH YOHANA

Posted on: November 29th, 2024

Hayawi hayawi hatimaye yamekuwa baada ya mchakato mrefu katika mbio za uchaguzi wa viongozi ngazi ya Serikali za Mitaa leo Novemba 29, 2024 viongozi waliochaguliwa na wananchi kuongoza Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Kufuatia uchaguzi uliofanyika Novemba 27, 2024 wamekula kiapo cha uaminifu na kutunza siri, utii na uadilifu mbele ya Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Nyarugusu Mhe Joseph P Kaguli.

Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Nyarugusu Mhe Joseph P Kaguli akiwaapisha Viongozi waliochaguliwa kuongoza Serikaliy za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Uapisho huo umefanyika katika ukumbi wa Amani na Upendo Kata ya Nyarugusu ambapo viongozi kutoka kata za Nyarugusu, Nyaruyeye, Nyakamwaga Rwamgasa na Busanda wamekula kiapo hicho ambapo Mhe Kaguli Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo amewataka viongozi walio kula kiapo kutokufanya mzaha na kiapo hicho katika kuwatumikia wananchi.

Viongozi waliochaguliwa na wananchi kuongoza Serikali za Mitaa wakila kiapo cha utii uadilifu na kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Nyarugusu Mhe Joseph P Kaguli


Viongozi wa Serikali za Mitaa wakila kiapo cha utii, uadilifu na kutunza siri Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Muchunguzi Mujuni katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Bugando

Akifungua kikao hicho cha kuwaapisha Viongozi hao Msimamizi Msaidizi ngazi ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Sarah Yohana amewapongeza viongozi hao kwa kupewa  dhamana ya kuwatumikia wananchi na kuwataka kuwa chachu ya kuendelea kuchochea shughuli za maendeleo.

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bi Sarah Yohana akiwaasa Viongozi waliochaguliwa kuongoza Serikali za Mitaa Wakati wa Kiapo kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Amani na Upendo Kata ya Nyarugusu

Zoezi la uapisho limefanyika katika maeneo mbalimbali Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo viongozi kutoka kata za Katoro, Nyamigota, Ludete, Magenge na Kaseme wameapa mbele ya Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Katoro Mhe Adam W.Mashiba.

Kwa upande wa viongozi kutoka kata za Nzera, Katoma, Izumacheli, Nyamboge,Lwezera,Nkome, Kakubilo, Bugulula, Senga na Nyawilimilwa  wamekula kiapo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi  Mahakama ya Wilaya ya Geita Mhe Muchunguzi Mujuni.

Viongozi waliochaguliwa kuongoza Serikali za Mitaa Novemba 27,2024 wakila kiapo mbele ya Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Katoro Mhe  Adam W.Mashiba Kata ya Katoro

Zaidi ya Viongozi 1657 wamekula kiapo leo katika maeneo tofauti ambapo wasimamizi wasaidizi wamewapongeza na kuwatakiwa  majukumu mema katika majukumu yao ya kuwatumikia wananchi.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa