• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

TIMU YA WATAALAM KUTOKA MKOA WA GEITA YAKAGUA NJIA YA MWENGE-GEITA DC

Posted on: July 26th, 2024

OCTOBA 5, 2024 Halmashauri ya Wilaya ya Geita inatarajia kupokea Mwenge wa Uhuru ambao utakimbizwa umbali wa km 45 kutoka eneo la mapokezi kata ya Bugulula hadi eneo la mkesha katika kata ya Nkome na km 34 kutoka kata ya Nkome hadi makabidhiano katika halmashauri ya Buchosa wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza na kufanya jumla ya km 79.6.

Katika kuhakikisha maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yanakuwa mazuri, kamati kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita ikiongozwa na Afisa mipango wa Mkoa wa Geita Ndg.Deodatus  Kayango Julai 25, 2024 imefanya ziara ya kukagua miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru ifikapo October 5,2024.

Timu ya Ukaguzi wa miradi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita ikikagua miradi ya maendeleo inayotarajiwa kutembelewa na Mwenge wa Uhuru Octoba 05, 2024 katika halmashauri ya Wilaya ya Geita Julai 25, 2024. Huu ni mradi wa shamba la miti unaomilikiwa na mtu binafsi. Shamba hilo lina ukubwa wa ekari 6 ambapo ekari 5 ndizo zimepandwa miti aina ya Pinus Caribea. Kauli mbiu ya Mwenge  wa Uhuru inasema “TUNZA MAZINGIRA NA SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA UJENZI WA TAIFA ENDELEVU”

Kamati hiyo imezunguka katika miradi yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakimbizwa ambayo ni Kata za Bugulula Mwenge wa uhuru utakapo pokelewa na kisha kuendelea katika kata za Nzera, Katoma,Nyamboge na mwisho kata ya Nkome ambapo kutakuwa na mkesha wa Mwenge wa Uhuru.

Mradi wa Maji kata ya Katoma wenye tanki lenye ujazo wa lita 225,000 ambapo unatarajiwa kutoa huduma kwa wakazi wapatao 11,609 kupitia vituo vya kuchotea na wateja wa majumbani

Mbio za Mwenge wa Uhuru zinatarajiwa kukagua miradi mbalimbali itakayozinduliwa na kuwekwa mawe ya msingi zikiwemo shule, zahanati,ofisi, miradi ya maji, barabara pamoja na klabu za kuzuia na kupambana na rushwa na dawa za kulevya.

Ukaguzi wa mradi wa barabara ya Lami nyepesi yenye urefu wa km 1.1 unaojengwa na TARURA

Aidha katika ukaguzi wa miradi hiyo Kayango amewasisitiza wahandisi na mafundi ujenzi wanaotekeleza miradi hiyo kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii na weledi ili kujenga miradi iliyo bora na kuepuka kujenga miradi iliyo chini ya kiwango.

Ukaguzi wa mradi wa zahanati ya Nkome. Timu hiyo imemtaka Mkandarasi kuongeza kasi ya ukamilishwaji wa mradi huo kwa kuhakikisha mafundi wanakuwa katika eneo la ujenzi (site)

Vilevile Kayango amewataka watendaji wa kata zote Mwenge wa Uhuru utapopita kuendelea kufanya hamasa ili wananchi wajitokeze kwa wingi katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.

Kikundi cha vijana (Masakuro) kata ya Nyamboge wanaoendesha mradi wa kukodi baiskeli ulioanzishwa kwa nguvu ya vijana na kuungwa mkono na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kupatiwa mkopo wenye riba nafuu ambapo kamati hiyo imekipongeza na kukitaka kuendelea kujituma kwa bidii zote ili kuweza kufikia malengo yao.

Mbali na hivyo kamati hiyo imekipongeza kikundi cha vijana (Masakuro) kata ya Nyamboge wanaoendesha mradi wa kukodi baiskeli ulioanzishwa kwa nguvu ya vijana na kuungwa mkono na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kupatiwa mkopo wenye riba nafuu.

“Muendelee kujituma kwa bidii zote ili kuweza kufikia malengo yenu na mnapokamilisha mkopo wenu muendelee kukopa ili kukuza kikundi chenu”,amesema Kayango

Kikundi hicho kimeishukuru halmashauri kwa kuwapa mkopo na kuahidi kuendelea kuchapa kazi pasipo kuchoka na kuweza kupata kile walichokusudia.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa