• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA SEDIT LAGAWA MASHINE ZA NAFAKA NA VIFAA MBALIMBALI KWA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI ILI KUKUZA UCHUMI KUANZIA NGAZI ZA FAMILIA

Posted on: August 18th, 2022

Na. Michael Kashinde

Shirika la SEDIT linaloshirikiana na PLAN International pamoja na Kivulini katika kutekeleza mradi wa kutokomeza ajira hatarishi na ukatili kwa watoto awamu ya Tatu mwaka 2020 - 2023 limegawa vifaa mbalimbali zikiwemo mashine za nafaka kwa vikundi mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita ikiwa ni mwendelezo wa harakati zake za kuchochea ukuaji wa kipato kuanzia ngazi ya familia.

Agosti 15, 2022  shirika hilo linalofanya kazi katika kata nne za Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambazo ni Nyamigota, Magenge, Nkome na Senga zenye jumla ya vijiji 15 limevifikia vikundi linavyovilea na kuvipatia vifaa hivyo kulingana na mahitaji ya vikundi husika.

Aidha vikundi vilivyofaidika na mgawo huo ni pamoja na Amani kutoka Senga waliopata mashine ya kupukuchua mahindi, Upendo kutoka Senga wakipatiwa mashine ya kusaga mahindi huku kikundi cha Amani kutoka Nkome kikipatiwa mashine ya kusaga karanga na siagi ya karanga.

Vikundi vingine ni pamoja na Vijana shupavu kutoka Senga waliopatiwa Seti ya vifaa vya kulishia kuku, Wajasiriamali makatani kutoka Nkome waliopatiwa Incubator, Nyikonga Magenge na Mabinti Shujaa kutoka Nyamigota waliopatiwa vyerehani viwili viwili kwa kila kikundi.

Vifaa vingine ilivyotolewa na Shirika la SEDIT ni pamoja na Embroider Machine, Grinder, pampu ya maji, mpira wa maji, na Mashine ya kufyatulia tofali huku thamani ya vifaa vyote vilivyotolewa ikiwa ni Tshs.14,878,500/= ambapo kati ya hizo kiasi cha Tshs. 12,944,700/= zimetolewa na mradi huku Tshs. 1,933,800/= zikichangwa na vikundi vitatu kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivyo.

Bw.Thoba John Mratibu wa mradi wa Utokomezaji wa ajira hatarishi na ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto awamu ya tatu akizungumza wakati wa kukabidhi baadhi ya vifaa hivyo katika kata ya Senga amesema kuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuna jumla ya vikundi 58 ambapo vikundi 12 vimepewa vifaa na mashine hizo ili kuungwa mkono kutokana na ubunifu na juhudi zao katika miradi mbalimbali ya vikundi kulingana na maeneo yao.

Aidha Bw. Thoba ameendelea kwa kusema kuwa kupitia vikundi hiyo vya hisa mradi umeweza kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali kupitia wawezeshaji jamii na kuwawezesha wanachama kuanzisha miradi ya mtu mmoja mmoja na pia imeanzishwa miradi mbalimbali ya vikundi ikiwa ni pamoja na ununuzi wa mazao, ulimaji bustani, ufyatuaji wa tofali, useremala, ufugaji wa kuku,ushonaji wa nguo na miradi mingine.

Kwa upande wake Afisa Maendeleleo ya jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bw. Novatus Bituro amewasihi wanavikundi waliopokea vifaa hivyo kuvitunza, kuvithamini na kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa huku akisisitiza kuwa ana Imani vifaa hivyo vikitumiwa kama inavyotakiwa vitakuwa chachu ya kukua kwa miradi ya walengwa kwa kuwa watajipatia kipato cha uhakika kitakachosaidia kukuza uchumi wa kaya zao.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa