• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

RAIS SAMIA AMWAGA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 9.2 GEITA DC UTEKELEZAJI WA MIRADI

Posted on: January 12th, 2025

WAJUMBE wa Kamati ya Siasa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilayani Geita wametembelea na kukagua utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 9,244,350,934 inayo tekelezwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akiongoza Kamati hiyo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Geita Komredi Barnabas Mapande amesema Serikali inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa awamu ya sita inaleta fedha nyingi kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na kuwataka wananchi kuendelea Kumuombea Mhe Rais kwa kazi kubwa anayoifanya.

“Serikali ya awamu ya sita inaleta fedha nyingi za Miradi katika maeneo yetu kwa ajili ya kuwahudumia Wananchi hivyo nitoe rai kwa Wananchi kuilinda Miradi inayotekelezwa katika maeneo yao." Amesema Komredi Barnabas.

Katika upande mwingine Kamati hiyo imepongeza hatua ya Diwani wa Kata ya Kakubilo, Mhe Kesi Gayo Nyanda, kwa kutoa eneo lake lenye hekari sita kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Ikigijo, iliyopo katika Kijiji cha Kikwete, Kata ya Kakubilo yenye thamani ya Shilingi

Mapande amesema hatua hiyo ya Mhe Diwani kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule ni ya kuigwa na viongozi wengine katika kuchangia maendeleo.

Pamoja na pongezi hizo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita, Barnabas Mapande, amesema ili dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kufanikisha miradi kwa wananchi inatimia Serikali haina budi kuhakikisha mafundi wanaosimamia miradi wanakuwa na vigezo stahiki.

Ziara hiyo iliyo fanyika kwa siku mbili Januari 9 na 10, 2025 imetembelea Miradi ya Afya, Elimu, Maji na miundombinu ya Barabara ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.


Kamati ya Siasa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Geita imetembelea Ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi Kituo cha afya Busanda wenye thamani ya Shilingi Milioni 114,946,545.00. Ujenzi wa nyumba hiyo umetekelezwa na kujengwa na  Mkandarasi DELTA MULTIHOLDINGS SOLUTION LTD na kusimamiwa kwa ushirikiano kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Mgodi wa Buckreef

Ujenzi wa Shule mpya ya Msingi  Bwawani kupitia mradi wa BOOST wenye thamani ya Shilingi Milioni 348,500,000.Shule hiyo inaenda kupunguza umbali wa wanafunzi kutembea umbali mrefu. Kamati ya Siasa imeipongeza Halmashauri kwa ujenzi wa shule hiyo katika kukabiliana na adha walizokuwa wakipata wanafunzi kutembea umbali mrefu.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilayani Geita Komredi Barnabas Mapande akimtua mama ndoo ya maji ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi  katika Mradi wa Maji wa Katoro-Buseresere wenye thamani ya Shilingi Milioni 6,617,314,331 wenye uwezo wa kuzalisha  zaidi ya lita za ujao 2,500,000 kwa siku na kuhudumia zaidi ya wakazi 120,000 kwa kata za Ludete, Nyamigota, Katoro na Buseresere.

Kamati ya Siasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ikikagua ujenzi wa Shule Mpya ya Ufundi ya Amali Kata ya Nyamigota kijiji cha Chibingo  yenye thamani ya Shilingi Milioni 584,280,029. Kamati hiyo imeitaka Halmashauri kuwanyima kazi mafundi janja janja wanaochelewesha kazi ili wasiharibu kazi na kupoteza dhamira ya Mhe Rais kuwaletea wananchi maendeleo.

Ujenzi wa mradi wa shule  mpya ya Sekondari Kakubilo kijiji cha Kikwete wenye thamani ya Shilingi Milioni 584,280,029 ambapo unatarajiwa kupunguza kwa kiwango kikubwa msongamano wa wanafunzi katika shule ya Sekondari Kakubilo

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa