• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

RUWASA YAAZIMIA KUPUNGUZA MAGONJWA YATOKANAYO NA UKOSEFU WA MAJI SAFI NA SALAMA.

Posted on: June 11th, 2024

Na: Hendrick Msangi

Wakala wa maji safi na usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA) wilayani Geita katika taarifa yake kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika May 9, 2024 makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeazimia kupunguza magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji safi na salama kama vile kuhara, homa ya matumbo na Kipindupindu.

Hayo yameelezwa katika Kikao cha baraza la madiwani wakati wa uwasilishaji wa utekelezaji wa shughuli za serikali ngazi ya Halmashauri na taasisi kwa kipindi cha robo ya tatu Januari hadi Machi 2024 ambapo katika taarifa yake, Injinia Sande Batakanwa ambaye ni Meneja Ruwasa Wilayani Geita imesema Ruwasa pamoja na kupunguza magonjwa hayo pia upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo mengi ndani ya Halmashauri umeokoa muda  uliokuwa unatumika  kufuata maji mbali na kupelekea kusimama kwa shughuli nyingine za uzalishaji.

Baadhi ya Madiwani katika kikao Cha baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakifuatilia Kwa umakini nyaraka za taarifa za Utekelezaji wa Shughuli za Maendeleo yaliyotekelezwa Kwa kipindi Cha Januari hadi Machi mwaka huu 2024.

Utekelezaji wa miradi hii umeendelea kutoa ajira kwa vijana wengi ndani ya Halmashauri ambapo Ruwasa imekuwa ikitumia nguvu kazi iliyopo maeneo miradi inapotekelezwa na kufungua fursa za kiuchumi.

Jumla ya kata 5 ambazo ni Nkome, Katoma, Nyamboge, Nzera na Lwezera zinapata maji safi na salama kutokana na maboresho yanayoendelea kufanyika na Wakala wa maji safi na Usafi wa mazingira (RUWASA)

Huduma ya maji vijijini kwa Wilaya ya Geita inapatikana kupitia vyanzo mbalimbali vya maji vikiwemo  visima vifupi (83) visima virefu (140) maji ya bomba toka Ziwa Viktoria na visima vya asili 130.

Wilaya ya Geita ina miradi ya mtandao 21 katika meneo mbalimbali ndani ya wilaya ambayo inatoa huduma za maji kwenye vijiji 26 na miradi ya pampu 148 inayotoa huduma kwenye vijiji 75. Miradi ya myandao ni pamoja na Chankorongo, Izumacheli, Mharamba, Nyamboge, Nzera,Nyakagomba, Luhula, Inyara, Njiapanda Inyara, Kasesa, Kaseme, Lwamgasa, Nyakagwe, Kamena, Ikina, Nyamalimbe, Katoma, Mawemiru, Nkome, Busanda na Katoro.

Katika taarifa hiyo, imeeleza jumla ya kiasi cha shilingi 1,881,029,138.40                                                                                            zimepokelewa kwa ajili ya miradi ya maji  huku fedha iliyotengwa katika bajeti ya mwaka 2023/2024 ni kiasi cha shilingi 3,240,232,481.13.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuleta fedha nyingi ili kutimiza dhamira yake ya kuhakikisha huduma ya maji safi na salama inapatikana katika kila kijiji ikiwa ni utekelezaji wa kampeni yake ya kumtua mama ndoo kichwani.


Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • GEITA DC YAANZA KWA KISHINDO SHIMISEMITA 2025, YACHAPA NETIBOLI, MPIRA WA WAVU NA SOKA!

    August 16, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA GEITA ATEMBELEA TIMU ZA HALMASHAURI SHIMISEMITA TANGA

    August 16, 2025
  • MORALI JUU: WACHEZAJI WA GEITA DC WAPANIA VIKOMBE VYOTE TANGA

    August 15, 2025
  • RAS-GEITA ATOA WITO WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025

    August 12, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa