• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

RC SENYAMULE AIPONGEZA GEITA DC KWA KUPATA HATI SAFI

Posted on: June 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kupata hati safi katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali CAG kwa mwaka wa Fedha 2021/2022.

Ametoa Kauli hiyo akiwa kama mwenyekiti katika kikao cha Baraza maalumu la  madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita kilichokaa Juni 23, 2022 katika ukumbi wa Halmashauri Nzera kwa ajili ya kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali CAG.

Mhe. Senyamule amesema Halmashauri zote za Mkoa wa  Geita zimefanya vizuri na kupata hati safi hali inayoupa heshima Mkoa wa Geita, huku akiipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kukusanya mapato mengi zaidi ya makadirio ya bajeti.

Aidha Mhe. Senyamule amewataka viongozi mbalimbali kuongeza juhudi na maarifa katika kusimamia miradi mbalimbali ili ikamilike kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa ili Kuendelea kumtia Moyo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akitoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ndani ya Mkoa wa Geita.

 Wakati huo huo Mhe. Senyamule ametumia nafasi hiyo kuwataka viongozi mbalimbali kusimamia suala la upatikanaji wa chakula mashuleni na kudhibiti utoro, huku akitoa wito kwa viongozi kuwahamasisha wananchi kushiriki zoezi la Sensa ya watu na makazi bila kusahau kuyatangaza maendeleo yanayofanywa na Serikali ya awamu ya sita.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo akizungumza katika kikao hicho amewataka wakaguzi wa ndani kushirikiana na wakuu wa Idara mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili awamu ijayo wapunguze hoja.

Wakati huo huo Mkaguzi Mkuu wa nje Mkoa wa Geita CPA Richson Ringo akizungumzia taarifa ya hoja hizo amewashauri Wakuu wa Idara na watumishi wote kwa ujumla kuzingatia sheria, kanuni, na taratibu za manunuzi ili kuepuka hoja, huku akiwataka idara ya manunuzi kuwa na kumbuumbu ya nyaraka zote zinazotakiwa katika manunuzi.

Katika kikao hicho cha Baraza maalumu la Madiwani Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg. John Paul Wanga alianza kwa kuwasilisha hoja zilizotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Charles Kazungu akizungumza katika kikao hicho amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita itafanya hima kuhakikisha inazifuta hoja za mkaguzi, huku akishauri kutolewa kwa fedha za kutosha katika mikopo ya makundi maalumu ili fedha hizo ziwe na tija kwa wanufaika.




Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa