• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

RAIS SAMIA AWAPA FURAHA WANANCHI GEITA DC ZAIDI YA BILIONI 1.2 KUTOLEWA MIKOPO

Posted on: February 10th, 2025

Nzera-Geita

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 689,000,000 ikiwa ni sehemu ya asilimia 10 ya mikopo inayotolewa na Serikali kwa makundi ya  watu wenye ulemavu, vijana na wanawake.

Akizungumza katika Hafla ya uzinduzi wa utoaji wa mikopo na vitambulisho vya wajasiliamali katika viwanja vya Halmashauri-Nzera, Februari 10, 2025, Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Komba amelipongeza Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa namna ambavyo wanaisimamia Halmashauri na kuweza  kutenga fedha hizo ili wananchi waendelee kunufaika.

Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda akizungumza katika hafla ya ugawaji mikopo Halmashauri ya Wilaya ya Geita

 “Kwa namna ya kipekee tumshukuru Rais wetu Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kurejesha mikopo kwa upendo wake na mapenzi makubwa aliyo nayo kwa Watanzania ili waweze kujikwamua kiuchumi.” Amesema Bi Lucy Beda.

Aidha Katibu Tawala huyo amewaasa wana vikundi wote walionufaika na mikopo hiyo kuendelea kuimarisha mahusiano kwenye vikundi na kuepuka migogoro ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea katika vikundi hivyo.

“Tujiepushe na migogoro, tuendelee kushikamana ili malengo ya mikopo yafikiwe na kila mmoja awe na taarifa sahihi za kikundi kujua nini kinaendelea” Amesisitiza Bi Lucy Beda.

Pamoja na hayo, Bi Lucy Beda ameongeza kwa kusema, Serikali imeviamini vikundi hivyo na kuwataka kuendelea kushikamana kwani Serikali imetoa mikopo isiyo na riba na kuwataka kufanya kazi kwa bidii ili waweze kurejesha fedha walizokopeshwa na kuepuka kuitumia mikopo hiyo kwenda maeneo mengine kukopa.

Vile vile Katibu Tawala huyo amewasihi wana vikundi hao kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili na wananchi wengine wenye sifa waweze kupata mikopo hiyo isiyokuwa na riba huku akisisitiza kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa.

Aidha Beda ametoa rai kwa Maafisa Maendeleo kwa ngazi ya kata kuvitembelea vikundi vilivyokopeshwa mara kwa mara ili kujua changamoto zozote wanazokutana nazo na kuzitatua kwa wakati na kuendelea kutoa elimu kwa ambao hawajapata mikopo hiyo  ili waweze kuomba mikopo  ya Serikali isiyokuwa na riba katika kutimiza adhma ya Dkt Samia ya kuwahudumia wananchi.

Itakumbukwa kuwa Serikali ilisitisha zoezi la utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Aprili 2023 kutokana na sababu mbalimbali zikiwepo namna ya uratibu wake na urejeshwaji wa mikopo hiyo na baadaye Septemba 2024 Serikali ilikamilisha uandaaji wa kanuni mpya na kuruhusu Mamlaka za Serikali za mitaa kuendelea na zoezi la kutoa mikopo.

Baadhi ya pikipiki ambazo zimetolewa mkopo kwa kundi la Vijana maarufu kama bodaboda

Kwa upande wake Ndg George Kitaba ambaye ni mnufaika wa mikopo hiyo kutoka kundi la Walemavu ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe DKT Samia Suluhu Hassan kwa kurejesha mikopo hiyo. “ Kikundi chetu cha Walemavu Msasa-Busanda ni mara ya tatu kuchukua  mkopo tulianza na milioni 6 na sasa tumepewa Milioni 20” Ameongea kwa furaha ndg George Kitaba.

Naye Bi Magdalena Andrea mwanakikundi kutoka Wanawake na Mendeleo –Kasota ambacho kinajishughulisha na shughuli za ufugaji ameishukuru Serikali kwa kutoa mikopo hiyo ambayo inawasaidia kuanzia ngazi ya familia na kusema kikindi hicho kimepokea kiasi cha Shilingi Milioni 20 ukiwa ni mkopo wao wa 5 tangu wameanza kukopa katika Halmashauri.

Jumla ya Vikundi 39 kati ya 47 vimekidhi vigezo vya kupewa mikopo hiyo  ambavyo wanawake ni vikundi 23, vijana vikundi 14 na vikundi vya watu wenye ulemavu 2 ambapo kiasi cha Shilingi Milioni 689,000,000 kimetolewa katika awamu ya kwanza.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa