• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA GEITA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: February 24th, 2024

Na Hendrick Msangi

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita Ndugu Nicolaus Kasendamila ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Halmashauri.

Pongezi hizo zimejiri baada ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Geita ilipofanya ziara yake Februari 23, 2024 kwa kutembelea mradi wa shule ya msingi Nyaluhama iliyopo kata ya Bugalama Tarafa ya Kasamwa yenye jumla ya wanafunzi 552 wavulana wakiwa 290 na wasichana 262.

Ujenzi wa shule ya Msingi Nyaluhama umegharimu jumla ya kiasi cha shilingi 540,300,000 kutoka serikali kuu-BOOST, mradi huo umekamilika kwa madarasa 2 ya shule ya awali, madarasa 14 ya shule ya msingi, jengo la utawala, vyoo matundu 24 na kichomea taka.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa kamati ya Siasa ya Mkoa, ambaye ndio Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita Ndugu Nicolaus Kasendamila aliitaka Halmashauri ya Kijiji kutafuta eneo kwa ajili ya uwanja wa michezo kwani ni muhimu kwa shule hiyo ambayo imejengwa katika ubora wa hali ya juu.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita Ndugu Nicolaus Kasendamila amewataka wananchi Wilayani Geita kuendelea kupendana kama ambavyo Mhe Rais anavyowapenda kwa kuwaletea maendeleo ya miradi mingi ya shule zenye ubora, vituo vya afya na zahanati na miundombinu mizuri ya barabara

Aidha Ndugu Kasendamila aliwataka watumishi kupendana kwa kuwa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anawapenda ndio maana analeta maendeleo Wilayani Geita.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ndugu Cornel L.B Magembe akizungumza na wanafunzi, walimu na wananchi wa kata ya Bugalama Tarafa ya Kasamwa ambapo amewasisitiza kuendelea kulipa kipaumbele swala la Lishe shuleni hapo ili wanafunze waweze kupata chakula wawapo shuleni

Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela alipongeza ukamilishwaji wa mradi huo wa shule ya Msingi Nyaluhama ambapo alisema dhamira ya Mhe Rais ni kuwaondolea wananchi adha kwa kuwapunguzia mzigo wananchi ndio maana analeta fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo.”Mmeonyesha uwezo mkubwa, mmetekeleza kwa vitendo ukamilishwaji wa shule ya msingi Nyaluhama” alisema Shigela.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela amesema dhamira ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuwaondolea wananchi adha kwa kuwapungizia mzigo kwa kuendelea kuleta fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa

Mradi mwingine ambao kamati hiyo ya Siasa Mkoa iliweza kuitembelea ni ujenzi wa nyumba ya watumishi 2in1 katika shule ya sekondari Nzera yenye jumla ya wanafunzi 260 ikiwa wavulana ni 122 na wasichana 138 huku walimu walio ajiriwa na serikali wakiwa 10.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nzera iliyopo kata ya Nzera ambayo ndio makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakifurahia ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Geita wakati wa kuangalia mradi wa Nyumba ya watumishi 2in1 iliyogharimu kiasi cha shilingi 100,000,000 kutoka serikali kuu kupitia mfuko wa SEQUIP 

Mradi huo wa nyumba ya watumishi 2in1 umegharimu kiasi cha Shilingi 100,000,000 kutoka serikali kuu kupitia mfuko wa SEQUIP ambapo familia mbili zipo tayari kuingia kwenye nyumba hiyo ikiwa ni juhudi za serikali ya awamu ya sita kuwawezesha walimu kufanya kazi katika mazingira mazuri

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nyaluhama iliyopo kata ya Bugalama wakiwa na furaha baada ya kutembelewa na Kamati ya Siasa Mkoa wa Geita ambapo wametakiwa kuweka bidii kwenye masomo

Wakihitimisha ziara hiyo, Mwenyekiti huyo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ndugu Karia Rajabu Magaro na kusema ujio wake umeleta chachu ya kukamilika kwa miradi ya maendeleo inayondelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Kamati ya Siasa Mkoa wa Geita ilitembelea Jengo la ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Geita lilipo kata ya Nzera ambapo walipongeza watumishi chini ya Mkurugenzi Mtendaji  kwa Kuhamia katika jengo hilo


Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • GEITA DC YAANZA KWA KISHINDO SHIMISEMITA 2025, YACHAPA NETIBOLI, MPIRA WA WAVU NA SOKA!

    August 16, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA GEITA ATEMBELEA TIMU ZA HALMASHAURI SHIMISEMITA TANGA

    August 16, 2025
  • MORALI JUU: WACHEZAJI WA GEITA DC WAPANIA VIKOMBE VYOTE TANGA

    August 15, 2025
  • RAS-GEITA ATOA WITO WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025

    August 12, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa