• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MVUA NA UPEPO MKALI ZA SABABISHA UHARIBIFU MKUBWA WA SHULE YA MSINGI KAGEYE-GEITA DC

Posted on: October 30th, 2023

Na: Hendrick Msangi 


Kufuatia upepo mkali na mvua kubwa zilizonyesha siku ya Ijumaa Octoba 27, 2023, zimesababisha uharibifu mkubwa kwa Shule ya Msingi Kageya iliyoko Kata ya Nyachiluluma Wilayani Geita.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndugu Karia Rajabu Magaro akiwa na wajumbe wengine wakiwepo walimu, Mhe Diwani , pamoja na Watalam kutoka Halmashauri walipotembelea Shule ya Msingi Kageye iliyoharibiwa kutokana na mvua kubwa na upepo mkali.


Akizungumza mbele ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo,  Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Lusato  Mashauri, alisema majira ya saa nne asubuhi  wanafunzi wakiwa darasani, mvua kubwa zilizo ambatana na upepo mkali ziliengua mapaa ya  madarasa matatu pamoja na ofisi ya Mkuu wa shule.


Hata hivyo hakukuwa na  madhara ya Kibinadamu yaliyojitokeza kutokana na mvua hizo zilzoambatana na upepo mkali kwani walimu walishirikiana kuwahamisha wanafunzi hao na kuwapeleka kwenye madarasa mengine.

Mvua kubwa na upepo mkali vyaharibu madara ya shule ya Msingi Kageye Wilani Geita.

Naye Diwani wa Kata ya Nyachiluluma Mhe Rosa Musa alimuomba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Karia Rajabu Magaro kuipa kipaumbele shule hiyo zinapokuja fedha za miradi." Tunaiomba Halmashauri kuzipa kipaumbele shule zilizo pembezoni kama shule hii ya Kageye" alisema Mhe Rosa.


Akikagua Uharibifu huo, Ndugu Karia Rajabu Magaro ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita alisema swala hilo linafanyiwa kazi kwa uharaka na kumtaka Diwani huyo kuendelea kuwahamasisha wananchi wa Kata hiyo kwa kujitoa kwa ajili ya shule hiyo wakati Serikali inaendelea kufanya taratibu za ukarabati wa madarasa yaliyoharibiwa.


Aidha Mkurugenzi alimuagiza Mhandisi wa Halmashauri hiyo kufanya ukarabati wa shule hiyo kwa uharaka ili wanafunzi hao ambao kwa sasa wanasoma kwa vipindi tofauti waweze kurejea katika utaratibu wao wa kawaida.


Shule ya Msingi Kageye iliyopo Kijiji cha Kageye kata ya Nyachiluluma Wilayani Geita ni shule kongwe iliyo anzishwa mwaka 1978  na kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 883 na Jumla ya Walimu 10. Kufuatia uharibifu huo shule hiyo imebaki na madarasa matatu  huku madarasa matatu pamoja na Ofisi ya Mkuu wa shule kuharibiwa na mvua hizo.


Serikali inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kutenga fedha nyingi kwa ajili Miradi ya shule katika halmashauri ya Wilaya ya Geita na tayari shule hiyo imetengewa jumla ya kiasi cha shilingi  milioni 37 kwa ajili ya kupaua na kukamilisha vyumba vitatu vya madarasa kutoka mfuko wa CSR.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa