Geita-Vijijini
Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Geita Juni 04.2025, wamefanya Ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa kupitia mapato ya ndani, wajibu wa kampuni kwa jamii (CSR GGML) Serikali Kuu na Wadau wa Maendeleo (Word Bank)
Katika Ziara hiyo wameelekeza Mafundi na Wasimamizi wa Miradi hiyo kuongeza kasi katika Ukamilishaji wa Miradi hiyo ili wananchi waweze kunufaika na miradi hiyo kwa wakati.
Akizungumza katika Ukaguzi wa Miradi hiyo, Kaimu Afisa Mipango Bi.Sweetnes Malagila amewataka wasimamizi wa miradi hiyo katika Kata kuvitunza vifaa vya ujenzi ili vitumike katika utaratibu mzuri pamoja na kuwataka mafundi wanatekeleza miradi hiyo kuongeza kasi ili miradi ikamilike kwa wakati.
Kwa upande wake Afisa Ardhi Mwandamizi Wakili Hongera Edward amewataka watendaji wa vijiji na walimu ambao miradi inatekelezwa maeneo yao kuyatunza Mazingira kwa kufanya usafi na kuotesha miti na kuendelea kuyatunza majengo ya Serikali.
Miradi Iliyotembelewa ni miradi ya Afya na Elimu ambapo inatekelezwa kupitia vyanzo vya fedha kutoka CSR GGML Milioni 122.6, Mapato ya ndani Milioni 115, Serikali Kuu Milioni 100, Benki ya Dunia kiasi cha Shilingi Milioni 426 na kufanya jumla ya kiasi cha Shilingi Milioni 763.6
Ziara hiyo imefanyika katika Kata za Nyamboge, Katoma,Nkome, Kakubilo na Kata ya Kagu jimbo la Geita Tarafa ya Bugando.
Utaratibu wa kutembelea mradi ni moja ya mpango kazi ambao Mkurugenzi Mtendaji Ndg Karia Magaro amewaelekeza Wakuu wa Idara na Vitengo kutembelea miradi inayotekelezwa ili kuendelea kutoa msukumo wa ukamilishaji wa Miradi hiyo na kuanza kutumika kwani adhma ya Serikali ni kukamilisha miradi ili kutoa huduma kwa wananchi.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa