• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA GEITA HASHIM KOMBA ASISITIZA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA ZA UMMA-GEITA DC

Posted on: July 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Abdallah Komba, Julai 22, 2024 amefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo tarafa ya Bugando kata ya Bugulula jimbo la Geita vijijini.

Akiwa kata ya Bugulula, Mhe. Komba ametembelea mradi wa shule  shikizi ya msingi Kigoma iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi na kufikia hatua ya maboma yenye thamani ya shilingi milioni 58,510,000 mapato yaliyotokana na makato ya asilimia 20 kutokana na polisi jamii wanaolinda  eneo la leseni ya uchimbaji ya mgodi wa dhahabu Geita (GGML) ambapo kijiji cha Bugulula hupokea shilingi 36,800,000.

Awali akimkaribisha kwenye kata hiyo, Diwani wa kata ya Bugulula Mhe.Lupuga Elisha  amemuomba Mkuu wa wilaya kuwaunga mkono juhudi za kuanzisha ujenzi wa shule ya msingi shikizi Kigoma kwa  kukamilisha vyumba 8 vya madarasa na ofisi 2 za walimu ili shule hiyo iweze kuanza kutumika ifakapo 2025.

Ujenzi wa shule shikizi ya Kigoma iliyo kata ya Bugulula ambayo imegharimu kiasi cha shilingi Milioni 58,510,000 nguvu za wananchi na mapato ya kijiji. Shule hiyo itaondoa  changamoto ya mlundikano wa watoto katika shule mama ya msingi Bugulula pamoja na  kupunguza  umbali kwa watoto wa vitongoji viwili vya kigoma  na migombani unaopeleka utoro na kukatiza masomo.

Kukamilika kwa shule hiyo kutaondoa changamoto ya mlundikano wa watoto katika shule mama ya msingi Bugulula ikiwa ni pamoja na  kupunguza  umbali kwa watoto wa vitongoji viwili vya kigoma  na migombani unaopeleka utoro na kukatiza masomo.

Wananchi wa kata Bugulula wakiwa kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba ambapo wamemuomba awasaidie kupata ardhi  kwa wakala wa Huduma za misitu Tanzania ( TFS ) kwa ajili ya kilimo kufuatia ongezeko la mahitaji katika kata hiyo

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro amesema Halmashauri kupitia mapitio ya bajeti itaangalia namna ya kuwezesha ukamilishwaji wa madarasa hayo.

Pamoja na kutembelea shule hiyo, Mhe. Komba ametembelea ujenzi wa ofisi ya kijiji cha Nyamilyango uliojengwa na wananchi kwa thamani ya shilingi milioni 8,359,000 ambapo ameiagiza ofisi ya Mkurugenzi kupitia idara ya Mipango , Maendeleo ya Jamaii na Utawala kuwasaidia wananchi kuibua miradi yenye kipaumbele.

Mradi wa ofisi ya kijiji cha Nyamilyango kata ya Bugulula kilichojengwa kwa nguvu za wananchi  kwa thamani ya shilingi 8.3 ambapo ameiagiza ofisi ya Mkurugenzi kupitia idara ya Mipango , Maendeleo ya Jamaii na Utawala kutimiza wajibu katika kuwasaidia wananchi kuibua miradi yenye kipaumbele na kuwa na msukumo ili isikae muda mrefu bila kukamilishwa

Katika ziara hiyo, Mhe. Komba amefanya mkutano wa hadhara ambapo amewataka watumishi wa umma kusimamia fedha  za serikali ili zifanye kazi iliyokusudiwa ili wananchi wapate huduma zinazostahili,  ambapo serikali inatoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo. “Watendaji msome taarifa za mapato na matumizi, sitacheka na mtumishi wa umma yeyote atakayecheza na  fedha za serikali”. Amesisitiza Mhe. Komba.

Kufuatia malalamiko ya wananchi juu ya uhaba wa ardhi ya kufanya kilimo, Mhe. Komba amewaagiza wakala wa Huduma za misitu Tanzania ( TFS )kuwaelimisha wananchi juu ya  matumizi ya ardhi  ambayo ipo kwenye hifadhi na sio kuwaacha kulima na kisha kuja kukata mazao yao na kuwataka kuwasaidia wananchi ili wapate maeneo katika utaratibu unaohitajika.” Nitoe rai kwa wananchi asiwepo mtu atakeyafanya kitu kinyume na taratibu za serikali” amesema Mhe. Komba.

Kuhusu swala la mikopo kausha damu ambayo imekuwa changamoto kubwa kwa wananchi, Mhe. Komba ameiagiza Idara Maendeleo ya Jamii ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita kutoa elimu kwa wananchi juu ya mikopo inayotolewa na serikali ili wanufaike nayo na kuwataka wananchi kujitokeza ili wanaufaike na mikopo hiyo isiyokuwa na riba.

Akijibu kero ya mifugo kuharibu mazao , Mhe. Komba ameugaiza uongozi wa kijiji kuweka sheria zitakazo epusha migogoro ya wakulima na wafugaji na kuwataka wafugaji  kuwaheshimu wakulima ili kuendelea kudumisha amani na utulivu.

Pamoja na hayo, Mhe. Komba amewasihi wananchi wa kata ya Bugulula kujitokeza kwenye uboreshaji wa daftari la mpiga kura ili kuboresha taarifa zao na kuwata viongozi wa chama na serikali kuendelea kuwahamasisha  wananchi juu ya umuhimu wa daftari la mpiga kura.

Wananchi wa kata ya Bugulula wakiwa kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Geita ambapo wameaswa  kujitokeza  kwa  wingi katika uboreshaji wa daftari la mpiga kura  ili waweze kurekebisha taarifa zao

Akihitimisha ziara hiyo, Mhe. Mkuu wa Wilaya amekemea vikali tabia ya wananchi wanaodhuru watu wenye ulemavu wa ngozi na kuwataka kuunganisha nguvu kupambana na tabia hiyo kwa kuwafichua wanaohusika na vitendo hivyo vya kikatili.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa