• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA GEITA AITAKA CSR KUBADILI MFUMO WA USIMAMIZI WA MIRADI

Posted on: March 14th, 2025

Geita, Machi 13, 2025 – Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, amesema ipo haja ya kubadili mfumo wa usimamizi wa miradi inayotekelezwa kupitia Mfuko wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), hasa miradi inayosimamiwa na Kampuni ya GGML, kutokana na changamoto ya ucheleweshaji wa utekelezaji wake.


Akizungumza wakati wa ziara yake katika kata ya Nyachiluluma, Komba alieleza kuwa miradi mingi ya CSR haikamiliki kwa wakati, hali inayoweza kuongeza gharama za ukamilishaji wake baadaye.


“Ipo haja ya kubadilisha mfumo wa maamuzi wa CSR. Miradi tunayokabidhiwa inapaswa kulindwa ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati, badala ya kuachwa bila usimamizi thabiti,” alisema Komba.


Aidha, Mkuu wa Wilaya aliwataka viongozi wa kata na vijiji kushirikiana kwa karibu na wananchi katika kusukuma mbele maendeleo.


“Sisi tulioajiriwa na serikali hatujaja kuwa juu ya wananchi, bali kuwasikiliza na kuhakikisha hakuna anayebaki na manung’uniko,” alisisitiza.


Katika hatua nyingine, Komba amewataka viongozi kuendelea kuimarisha ulinzi shirikishi, ikiwa ni pamoja na vikundi vya sungusungu, ili kulinda amani na utulivu wa jamii. Pia, ametoa siku 14 kwa wasimamizi wa vituo vya maji waliokusanya fedha za wananchi lakini hawajalipa kwa mamlaka husika kuhakikisha wanarejesha fedha hizo ili huduma ya maji iendelee kupatikana bila kikwazo.


Kuhusu masuala ya mikopo, Mkuu wa Wilaya amewasihi wananchi kuepuka mikopo yenye riba kubwa inayojulikana kama kausha damu, akimtaka Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri kuhakikisha fedha za serikali zinazotolewa kwa riba nafuu zinawafikia wananchi waliotimiza vigezo.


Ziara ya Mkuu wa Wilaya inaendelea katika maeneo mbalimbali ya Tarafa ya Butundwe kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi.

Tangazo

  • HIZI HAPA AJIRA ZA KUMWAGA GEITA DC July 15, 2025
  • TANGAZO LA KUKODI MAGARI August 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 02, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TIMU YA MENEJIMENTI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA YARIDHISHWA NA KASI YA UKAMILISHAJI WA MIRADI

    October 17, 2025
  • GEITA DC KUENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA BOOST YENYE THAMANI YA BILIONI 3.2

    October 09, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NYANG'WALE ATEMBELEA BANDA LA MAONESHO YA MADINI LA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

    September 24, 2025
  • WAUGUZI WA AFYA NA MAAFISA LISHE GEITA DC WAASWA KUEPUKA MIGOGORO MAENEO YA KAZI.

    September 22, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa