• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA GEITA AHIMIZA HUDUMA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU

Posted on: March 12th, 2025

Geita, Tanzania 

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, ametoa wito kwa viongozi wa Kijiji cha Busaka na wakazi wake kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata huduma stahiki na msaada kutoka kwa wadau mbalimbali.

Mhe. Komba aliyasema hayo akiwa katika ziara yake ya kawaida katika Kata ya Bukondo, ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake katika Tarafa ya Butundwe. “Mnapoona kuna watoto wenye uhitaji maalumu, muwafikie na kuwahudumia ili kwa kushirikiana na wadau, tuweze kuwasaidia,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe Hashim Abdallah Komba akizungumza na wananchi katika ziara yake Tarafa ya Butundwe Halmashauri ya Wilaya ya Geita 

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya alisikiliza na kutatua kero mbalimbali, ikiwemo changamoto ya walimu wanaoishi mbali na shule, jambo linalosababisha uchelewaji wa vipindi darasani. “Hatuwezi kuwa na nyumba za walimu halafu walimu wakae mbali na vituo vya kazi. Lazima tuhakikishe wanakaa karibu ili waweze kuwajibika ipasavyo,” alisema.

Aidha, Mhe. Komba alisifu juhudi za serikali katika kusambaza umeme na kuwataka wananchi waendelee kuiamini serikali katika kukamilisha mpango wa usambazaji umeme kwa vijiji vyote vya Halmashauri.

Miradi Iliyotembelewa

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya alitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na:

•Zahanati ya Kijiji cha Chankolongo – Mradi huu umejengwa kwa nguvu za wananchi na fedha za Halmashauri, ukiwa katika hatua ya boma. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri aliahidi kuwa fedha zitatolewa kwa wakati ili kukamilisha ujenzi huo.

Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ikiendelea katika Tarafa ya Butundwe Halmashauri ya Wilaya ya Geita

•Chanzo cha maji cha Chankolongo – Baada ya wananchi kulalamikia upungufu wa maji licha ya chanzo kuwepo kijijini, Mhe. Komba aliiagiza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA) kukagua vituo vyote tisa vya maji na kuhakikisha vinafanya kazi ipasavyo. Pia alimtaka Afisa Tarafa kuandaa mkutano wa uhamasishaji kwa wananchi kuhusu usimamizi wa vituo vya maji.

•Zahanati ya Kijiji cha Kitigiri – Mhe. Komba alisisitiza umuhimu wa kuweka vipaumbele ili kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo kwa haraka.

•Elimu ya Afya juu ya Empox – Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri, Dkt. Modest, aliwapa wananchi elimu kuhusu ugonjwa wa Empox, akihimiza tahadhari kwa kuepuka kugusana na majimaji ya mwili kama mate na jasho, pamoja na kunawa mikono kwa maji yanayotiririka mara kwa mara.

•Ujenzi wa madarasa – Mkuu wa Wilaya alikagua maendeleo ya vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Lulama, vyumba saba vya madarasa katika Shule ya Msingi Nyasalala, na vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Busaka. Alisisitiza umuhimu wa mamlaka husika kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati.

Mhe. Komba aliendelea kuwasihi viongozi na wananchi kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, huku akiahidi kufuatilia utekelezaji wake ili kuhakikisha changamoto za wananchi zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa