• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA WA GEITA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA KWA USHIRIKIANO WAKE MZURI NA WAHISANI

Posted on: August 26th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh.Rosemary sitaki Senyamule,ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wawekezaji, katika kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ameyasema hayo Agosti 25 akiwa katika shule ya sekondari Evarist alipokuwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ambapo amesema kuwa mahusiano mazuri kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita na wawekezaji, ndio yanayofanikisha kuendelea kwa miradi hiyo. 

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh.Rosemary Senyamule (katikati) baada ya kukagua baadhi ya majengo katika shule ya Sekondari Evarist kutoka (kushoto) Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita John Paul Wanga akifuatiwa na diwani wa kata ya Nyarugusu Mh.Swalehe Juma Msene,(kutoka kulia )Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mh.Hadija Said Joseph.

Pongezi hizo zimekuja mara baada ya Mh.Senyamule kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Evarist, iliyojengwa na mwekezaji ambaye ni mchimbaji wa madini ya dhahabu katika kata ya Nyarugusu Bw.Evarist Paschal,kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kupitia mapato ya ndani,mradi wa CSR,nguvu za wananchi na mfuko wa jimbo.

Baadhi ya majengo mapya ya vyumba vya madarasa yaliyojengwa katika shule ya Sekondari Evarist. 

Aidha amempongeza pia Bw.Evarist kwa mchango wake huo wa zaidi ya milioni 138, huku akitoa wito kwa wachimbaji na wadau wengine wa maendeleo, kuendelea kujitolea kusaidia katika miradi ya maendeleo kwa faida ya jamii.

Jengo la utawala katika shule ya Sekondari Evarist likiwa katika hatua za mwisho kuelekea kukamilika  

Wakati huo huo Mh.Senyamule amewataka wanafunzi wa shule ya Sekondari Evarist ambao ndio wanufaika wa kwanza wa mradi huo, kuitunza miundo mbinu hiyo na kusoma kwa bidii, ili wapate matokeo mazuri, suala linalotazamiwa kama matokeo chanya ya miradi kama hiyo.

Ujenzi wa mradi huo wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 251 umeanza April 2021, ikiwa ni mkakati wa kupunguza msongamano mkubwa wa wanafunzi katika shule ya sekondari Nyarugusu, ambapo mpaka sasa tayari vyumba sita vya madarasa na ofisi mbili zimekamilika.

Jiwe la msingi la shule ya Sekondari Evarist

Aidha jengo la utawala,vyoo vya walimu na wanafunzi,na maabara ,vyote viko katika hatua za mwisho za kukamilika, huku kisima kikiendelea kujengewa ambapo pia mabweni tu ndio bado hayajaanza kujengwa.

Mkuu wa Mkoa Wa Geita Mh.Rosemary Senyamule akisalimiana na baadhi ya wakuu wa idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita alipowasili katika shule ya Sekondari Evarist


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa