• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA AWEKA WAZI VIPAUMBELE ANAVYOTAMANI KUVITEKELEZA AKIWA GEITA

Posted on: August 12th, 2021

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita John Paul Wanga amelishauri baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Geita kufikiria kuwasaidia wachimbaji wadogowadogo kwa kujenga vyuo vya Veta vitakavyokuwa vinafundisha stadi za uchimbaji wa madini ili kuwasaidia vijana kuwa na ujuzi wa shughuli hizo.

John Wanga ameshauri hayo leo Agosti 12, 2021 wakati akihutubia baraza la madiwani kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake kuwa mkurugenzi wa wilaya ya Geita,ambapo ameweka wazi vipaumbele 14, ambavyo atajielekeza yeye kama mkurugenzi na watendaji wake kuvitekeleza.

Baada ya kupokea taarifa kutoka kwa madiwani kuwa Zaidi ya kata 10 katika wilaya ya Geita zinajihusisha na uchimbaji wa madini ya dhahabu, amesema kuwa kuwapa elimu na ujuzi sahihi wa shughuli hizo, kutaisaidia Halmashauri ya wilaya ya Geita, kuwa na mapato ya kutosha kutokana na uchimbaji wenye tija,huku akiwataka madiwani kuwa na mawazo kama hayo ili kuwasaidia wananchi.

Amesema kuwa atahakikisha Halmashauri inawawezesha wananchi kiuchumi kwa kutoa mikopo amabayo ni asilimia 10 ya mapato ya ndani, kwa makundi maalumu kama vijana, wanawake na watu wenye ulemavu,ambapo fedha zote zitakazotolewa zinatakiwa kuzunguka kwa wahusika na kurejeshwa,huku akieleza kuwa ni vyema ikagawiwa fedha nyingi kwenye kikundi cha watu ili fedha hizo za mikopo zilete matokeo kwa wananchi kitu ambacho hata viongozi wengine wa juu wanatamani kukiona. 

Aidha mambo mengine ya kujielekeza katika utumishi wake aliyoyaeleza,ni pamoja na utawala,kukusanya mapato ya ndani,kukuza kilimo,uvuvi,mifugo,upimaji wa ardhi ili kuwa na makazi bora,kuboresha elimu na afya.

Mengine ni pamoja na kuimarisha usafi wa mazingira kuanzia ngazi za chini,kuboresha na kujenga miradi ya maji ili wananchi wapate maji safi na salama ,ujenzi wa majengo na barabara,miradi mikubwa ya vielelezo,na nishati ya umeme huku akisisitiza kuwa ‘wakandarasi wazembe hawana nafasi katika wilaya hii’

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAHIMIZWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU-CPA AMOS MAKALLA

    May 20, 2025
  • RUSHWA NI JANGA LINALOATHIRI MAENDELEO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KISIASA NCHINI-RAS GOMBATI.

    May 13, 2025
  • GEITA YAPATA MAJIMBO MAPYA YA UCHAGUZI.

    May 12, 2025
  • ALAT MKOA WA GEITA WAMPONGEZA MKURUGENZI GEITA DC USIMAMIZI MZURI WA MIRADI

    May 10, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa