• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI GEITA DC KARIA RAJAB AZINDUA MATOKEO YA UPIMAJI YA MITIHANI YA KITAIFA NA KUTOA TUZO KWA WALIMU WAKUU AMBAO SHULE ZAO ZIMEFANYA VIZURI

Posted on: October 3rd, 2023

Na: Hendrick Msangi

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndugu Karia Rajabu Magaro, amezindua  matokeo ya  Upimaji ya mitihani ya Kitaifa  katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na kukabidhi tuzo na zawadi kwa shule zilizo fanya vizuri na zile zilizofanikiwa kuongeza ufaulu katika mitihani hiyo (PRE NECTA MKOA)  kwa Mwaka 2022  kwa mitihani ya kidato cha pili (FTNA), kidato cha nne ( CSEE) na Kidato cha sita (ACSEE) kwa mwaka 2023. 


Awali akitoa taarifa ya seksheni ya elimu sekondari kwa Mkurungezi katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri  na kuhudhuriwa na wakuu wa shule za sekondari zilizopo katika Halmashauri hiyo, Kaimu Afisa Elimu Sekondari ndugu Richard Makoye alisema Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa sasa ina jumla ya Sekondari  75 ambapo 71 ni za serikali huku 4 zikiwa shule binafsi (Private schools)Aidha katika taarifa hiyo ilisema shule za serikali zina jumla ya wanafunzi 39,194 ambapo wavulana ni 20, 823 na wasichana idadi ikiwa ni 18,871, na kwa upande wa shule binafsi , wavulana ni 273 na wasichana ni 250 kufanya jumla ya wanafunzi 523 kwa shule binafsi. 

Kwa upande wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ni 78, ambapo wasichana 34 huku wavulana wakiwa 44.


Pamoja na hayo Makoye alimueleza Mkurugenzi kuwa idara ya elimu inaishukuru Serikali kwa kutenga fedha nyingi kwa ajili ya Miradi ya ujenzi wa mindombinu ya shule za sekondari Butundwe ambayo ujenzi wa vyumba vya madarasa 8, mabweni mawili, matundu 13 ya vyoo  ambapo gharama za fedha zilizo pelekwa kwa  miundo mbinu hiyo ni kiasi cha shilingi 487,300,000Ujenzi mwingine ambapo fedha zimepelekwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba ya mtumishi 2 in 1 katika shule ya sekondari Nzera wenye thamani ya shilingi 100,000,000, nyumba ya mtumishi 2 in 1 shule ya sekondari Samia Suluhu wenye thamani ya shilingi 100,000,000, Madara 8 kwenye shule mpya kata ya Ludete wenye thamani ya shilingi 200,000,000, jengo la utawala, Tehama, Maktaba, Maabara(3) , matundu ya vyoo 8 wenye thamani ya shilingi 377,069,467, Ujenzi mwingine ni wa shule mpya kata ya Isulwabutundwe wenye thamani ya shilingi 577,069,467Akieleza hali ya ufaulu kwa Matokeo hayo Kaimu  Afisa Elimu Sekondari ndugu Makoye alisema  kiwango cha ufauli  kwa mitihani ya Taifa kidato cha nne mwaka 2022 kimeongezeka toka asilimia 76.5 kwa mwaka 2021 na kufika asilimia 77.5 ambapo shule zilizofanya vizuri katika mitihani hiyo kwa mwaka 2022 ni pamoja na Shule ya sekondari Lutozo, Bugalama, Nkome  huku shule zilizofanikiwa kuongeza ufaulu ni  sekondari ya Nyaruyeye, Busanzu na BujulaAkiendelea kutoa taarifa hiyo kwa Mkurugenzi, Afisa elimu huyo alisema kwa upande wa mitihani ya upimaji wa kidato cha pili (FTNA) jumla ya Shule za sekondari 46 zilishiriki huku ufaulu ukiwa ni asilimia 86.7 ukishuka kwa asilimia 6.3 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2021 ambao ulikuwa asilimia 93. 


Shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya upimaji wa kidato cha pili (FTNA) ni pamoja na Nyamalimbe, Magenge na Bugalama huku shule zilizofanikiwa kuongeza ufaulu katika mitihani hiyo ni shule ya Sekondari Lwemo, Nyamalinde na BusandaAkipokea taarifa hiyo, Magaro ambaye ni Mkurugenzi Halmashauri ya wilaya ya Geita, aliwapongeza wakuu hao wa shule ambao shule zao zimeongeza kiwango cha ufaulu katika mithani hiyo.

 “Natambua zipo shule bado hazifanyi vizuri ninawagiza sasa muongeze jitihada katika usimamizi wa shule zenu.

 Tafiti mbalimbali zinaeleza wazi kuwa moja ya sababu za shule kufanya vizuri au vibaya ni aina ya uongozi uliopo katika shule husika” alisema Magaro.


Aidha aliwataka wakuu hao wa shule kuwa na ushirikiano katika utendaji wao na kuongeza juhudi katika utendaji ili kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka  huku akiwataka kuwa viongozi wazuri wakisimamia shughuli zote za kiuendaji katika shule zao ikiwa ni pamoja na miradi inayoendelea. 

“Halmashauri itaendela kushirikiana na nyie  kuwapa Motivation  kwa walimu ambao wataleta matokeo mazuri katika shule zao” Alisema Mkurugenzi huyo.

Katika halfa hiyo, ndugu Magaro alitoa maelekezo kwa wakuu hao wa shule  katika utendaji wa shughuli zao ambapo aliwataka kuhakikisha wanapokea na kutekeleza maelekezo ya Serikali ikiwemo uwasilishaji wa taarifa kwa wakati, kufuata sheria na miongozo na taratibu katika usimamizi wa shule.

Akiendelea kutoa maelekezo hayo, Magaro aliwataka wakuu hao wa shule kuisimamia miradi inayotekelezwa katika shule zao huku wakihakikisha majengo na mali za shule zinatunzwa vizuri.

 Pia aliwataka wawe na mahusiano mazuri na jamii inayowazunguka katika utendaji kazi wao pamoja na kuwa walezi na washauri wazuri kwa wanafunzi wanao wasimamia na  kuwataka kuhakikisha mwaka ujao wa masomo ufaulu unaongezeka.

 “Hakikisheni mnaanzisha masomo ya uchaguzi kwa wanafunzi kwa ajili ya kuwapanulia wigo wa ufaulu ikiwemo somo la Literature in English” alisema Magaro.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inamshukuru Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa shule za Sekondari .



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa