• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI GEITA DC ATOA WITO WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO INAYOTOLEWA NA SERIKALI

Posted on: February 10th, 2025

Nzera-Geita

MKURUGENZI Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro ametoa rai kwa wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuchangamkia fursa ya Mikopo isiyokuwa na riba inayotolewa na Serikali ya awamu ya Sita kupitia Halmashauri.

Magaro ameyasema hayo katika uzinduzi wa utoaji wa mikopo na vitambulisho vya wajasiliamali ulio fanyika katika viwanja vya Halmashauri-Nzera Februari 10, 2025.

“Ni faraja kubwa kwa Halmashauri kutekeleza hatua hii muhimu ya Serikali ya kutoa mikopo ya asilimia 10. Muongozo wa Serikali unasema kila bajeti ya mwaka tutenge fedha za miradi ya Maendeleo na fedha za Mikopo ya vikundi vya wanawake vijana  na watu wenye ulemavu " Amesema Magaro.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro akizungumza na wananchi waliojitokeza katika hafla ya utoaji mikopo.

Aidha Ndg Magaro amesema Halmashauri  imetenga Kiasi cha Shilingi Bilioni 1.2 kwa ajili ya wananchi ambao watakidhi vigezo  vya  kupata mikopo hiyo.

“Leo tuna toa Mikopo ya kiasi cha Shilingi Milioni 689,000,000 ikawe  hamasa  kwa wana kikundi wengine kujitokeza kuja kukopa" Amesema Ndg Magaro.

Wananchi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa katika viwanja vya halmashauri wakati wa hafla ya ugawaji mikopo.

Pamoja na hayo  Magaro ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayo ongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utaratibu mpya aliouweka wenye uwazi kusimamia mikopo hiyo.

“Niwaombe wote  mlionufaika na mikopo muweze kuandika kila mnachokifanya katika biashara  zenu ili Wataalam watakapopita kuwatembelea waweze kuwapa ushauri"

Vilevile Magaro ame wasihi wana vikundi hao kuhakikisha wanatoa taarifa Pale wanapopata changamoto kwa  kuwashirikisha Wataalam kutoka Halmashauri ili waweze kuwakwamua kwani Halmashauri ipo tayari wakati wote.

"Tuna amini kuwa mtakuwa chachu kwa kuhakikisha makubaliano yale mnayoyafanya mnayatekeleza kwenye miradi yenu mliyofungua na kusimamia marejesho kufanyika kwa wakati ili wananchi wengine  waweze kunufaika na mikopo hii" Ameongeza Magaro.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu ameishukuru  serikali kwa kurejesha mikopo hiyo toka Septemba 2024.

“Sisi Madiwani kazi yetu kubwa ni kusimamia na kuhakikisha fedha inatengwa kwa taratibu zilizowekwa kwa kila bajeti. Halmashauri itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya mikopo ya makundi ya wanawake vijana na watu wenye ulemavu” Amesema Mhe Kazungu

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu akizungumza na wananchi katika hafla ya utoaji mikopo

Vilevile Mhe Kazungu amevitaka vikundi hivyo kuitumia mikopo hiyo katika malengo yaliyokusudiwa ili kuweza kurejesha kwa uaminifu na kupelekea kupunguza idadi ya vijana walio mtaani kwa kujikwamua kiuchumi.

“Ni wasihi mkawe waaminifu kurejesha mikopo ili kuendelea kutoa fursa kwa wana Geita wengine kupata mikopo hiyo na mkawe kielelezo kizuri kwa wengine” Amesema Mwenyekiti

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilayani Geita Komredi Michael Msuya  ametoa wito kwa Halmashauri na Taasisi za umma kuwapa  fursa wana vikundi hao pale ambapo kuna kazi wanazoweza kuzifanya zikiwepo usambazaji wa chakula katika shule zinazohitaji chakula, shughuli za useremala na nyinginezo ili waweze kurejesha mikopo hiyo kwa wakati


Msuya amesema ili tija ya Mama Samia Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa itimie ni wajibu kwa maafisa maendeleo kuwasimamia wana vikundi hao ili waweze kutimiza malengo ya vikundi vyao.

Hali kadhalika Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Jonas Kilave amesema katika hafla hiyo kuwa jumla ya vikundi 39 vimekidhi kupata Mikopo ambapo vikundi vya wanawake 23 vimepatiwa kiasi cha shilingi Milioni 351, vikundi vya vijana 14 kiasi cha shilingi milioni 293 na vikundi vya watu wenye ulemavu 2 vikipewa kiasi cha shilingi milioni 45 na kufanya jumla ya kiasi cha shilingi milioni 689 kutolewa.


Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Jonas Kilave akiwasilisha taarifa ya utoaji wa mikopo kwa Halmashauri

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa