• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI GEITA DC APONGEZWA MAKUSANYO YA TSH BILIONI 11.9 MAPATO YA NDANI BAJETI 2025/26

Posted on: February 8th, 2025

Katika Mkutano wake Maalum uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita-Nzera, Februari 7,2025, Baraza la Madiwani limempongeza Mkurugenzi Mtendaji Ndg Karia Rajab Magaro kufuatia mapendekezo ya kukusanya Kiasi cha Shilingi Bilioni 11.9 mapato ya ndani.

Akizungumza katika Baraza Hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Charles Kazungu  amesema  Halmashauri imepata Mkurugenzi mtu bingwa na kupongeza  uaandaji mzuri wa Bajeti hiyo ya 2025/2026.

"Kitu kikikosewa kwenye maandalizi lazima kilete mkanganyiko mkubwa sana.  Nawapongeza sana ukiangalia bajeti  tuliyo nayo ya Bilioni 8.3 na sasa  tunaenda bajeti ya Shilingi Bilioni 11.9" Amesema Mhe Kazungu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Ndg Karia Magaro  amelishukuru Baraza hilo pamoja na ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa Ushirikiano mzuri ambao  umepelekea Halmashauri kufikia Bajeti hiyo.

Magaro ameongeza kwa kusema alipoingia Halmashauri alikuta Bajeti ya Halmashauri ni Kiasi cha Tsh Bilioni 5 baadaye Kiasi hicho kimeongezeka kwa kufika Bilioni 6 kwa mwaka wa fedha 2023/24 na mwaka  wa fedha 2024/25 kufika Bilioni 8 na sasa kuelekea 2025/26 Halmashauri inatarajia kufikia Bilioni 11.9 mapato ya ndani.

"Nakupongeza Mwenyekiti wa Halmashauri na baraza lako kwa namna ambavyo tumefanya kazi kwa kushirikiana kupitia Wataalam,  Watumishi kwani hii sio kazi ya mtu mmoja, Nilipokuja tulikuta Bajeti  ya Bilioni 5 na baadaye ikaendelea kuongezeka kuwa Tsh Bilioni  6.4 tukavuka lengo  na kwa mwaka wa fedha 2023-2024 bajeti ikawa Bilioni 7 na 2024 -2025 tukaenda  Bilioni 8 na sasa kwa mwaka wa fedha 2025/2026 tunazungumzia bajeti ya Shilingi Bilioni 11.9." Ameongeza Ndg Magaro.

Aidha Ndg Magaro  amewasihi Waheshimiwa Madiwani kuendelea kutoa ushirikiano kusimamia mapato ili adhma ya Halmashauri iweze kutimia kwa kuwa Bajeti hiyo imelenga kuwahudumia wananchi.

" Rais wetu anasisitiza tuweze kukusanya mapato ili Halmashauri ziweze kujitegemea kwa kiasi kikubwa" Amesema Ndg Magaro

Naye Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda ametoa wito  kwa Halmashauri kuendelea kuvisimamia vyanzo vya mapato vilivyopo ikiwa ni pamoja na Kuendelea kuongeza vyanzo vingine ili mapato yaendelee kuongezeka.

" Niipongeze Halmashauri kwani kwa Bajeti ya 2024/2025 malengo yalikuwa ni kukusanya Kiasi cha Shilingi Bilioni 8.3 na mpaka sasa kufika asilimia 58.3 hayo ni  mafanikio makubwa ".Amesema Bi Lucy Beda

Aidha Bi Lucy Beda ametoa wito kwa Waheshimiwa Madiwani kuendelea kuisimamia vema Halmashaur ili malengo ya Bajeti hiyo yaweze kutimia kwa kuwa inaenda kuyagusa wananchi.

Baraza hilo limeidhinisha  Rasimu ya mapendekezo ya bajeti Kiasi cha Shilingi Bilioni 93.5 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 huku TARURA wakiwasilisha Mpango wa Bajeti kiasi cha Shilingi Bilioni 5.1,  RUWASA Shilingi Bilioni 11.7 na kufanya Halmashauri kuwa na Rasimu ya mapendekezo ya bajeti kuwatumikia wananchi kiasi cha Shilingi Bilioni 110.4

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI. June 05, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU MKOA YATEMBELEA YATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA, GEITA.

    June 24, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 50 ZATUMIKA KUKAMILISHA MIRADI GEITA 2020-2025.

    June 21, 2025
  • RAISI DKT. SAMIA AZINDUA DARAJA LA KIGOGO-BUSISI.

    June 19, 2025
  • WATUMISHI WILAYANI GEITA WAKUMBUSHWA SUALA LA KUJIFANYIA TATHMINI.

    June 18, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa