• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI AWASHUKIA WAZABUNI WANAOKWAMISHA MIRADI

Posted on: November 19th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Ndg Karia Magaro Novemba 18, 2024 ameongoza timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya Geita kukagua miradi ya maendeleo katika kata za Nyamigota, Ludete na Katoro zilipo jimbo la Busanda.

Timu hiyo imetembelea na kukagua ujenzi wa shule ya amali iliyopo kata ya Nyamigota kijiji cha Chibingo mradi wenye thamani ya Shilingi Milioni 584,280,029 ili kuona hali halisi ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Amali ambaye pia ni Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Nyamigota Mwl Renatus Martini (wa pili kulia) akitoa maelekezo ya maendeleo ya mradi Mbele ya Timu ya menejimenti ya Halmashauri iliyoongozwa na Mkurugenzi mtendaji Ndg. Karia Magaro 


Aidha timu ya menejimenti imetembelea mradi wa upanuzi wa miundombinu ya kidato cha 5 na 6 shule ya sekondari Kagega wenye thamani ya shilingi Milioni 481, upanuzi wa miundombinu ya kidato cha 5 na 6 shule ya sekondari Lutozo mradi wenye thamani ya shilingi Milioni 381 na mradi wa shule ya msingi mtaa wa afya ambayo ilianza kwa nguvu za wananchi na baadaye kuendelezwa madarasa 9 kwa mfuko wa BOOST kwa thamani ya Milioni 351.5.


Timu ya menejementi ya Halmashauri ikikagua mradi wa ujenzi wa nyumba za waalimu katika shule ya Kagega iliyopo kata ya Ludete


Mwonekano wa madarasa katika mradi wa Upanuzi wa kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari Lutozo

Pamoja na miradi hiyo, timu iliweza kutembelea Kata ya Katoro eneo ambalo litajengwa shule ya sekondari ya kata ambapo kwa sasa ipo hatua za awali. Mradi huo una jumla ya kiasi cha shilingi Milioni 584,280,029.

Katika ukaguzi wa miradi hiyo timu ilibaini kuwepo kwa changamoto zinazosababishwa na wazabuni kwa kuchelewesha vifaa vya ujenzi kwenye miradi na hii ni kutokana na wazabuni hao kushinda tenda katika maeneo mengi ilihali hawana uwezo wa kusambaza vifaa kwa wakati.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita akikagua ubora wa tofali katika mradi unaendelea kujengwa shule ya sekondari Lutozo.


Kufuatia changamoto hiyo, timu ya menejimenti iliwafuatilia wazabuni hao na kuwapa muda maalum wa kuhakikisha vifaa vya ujenzi vinafika kwenye miradi ili mafundi ujenzi waweze kuendelea na kazi na miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuanza kutumika kama ambavyo mikataba ya ujenzi inavyowataka.

“Hizi kazi ni za Halmashauri hivyo niwatake mnapotangaza tenda kwenye mfumo wa Nest muangalie uwezo wa wazabuni katika kukamilisha kazi wanazoziomba katika Halmashauri ili kuepusha kuchelewesha miradi” amesema Magaro

Fundi Deogratius Wilson ni mmoja wa mafundi wanatekeleza miradi iliyotembelewa  na timu ya menejimenti ambapo amesema wanatumia muda mwingi kuwepo uwandani (site) bila ya kuwepo kwa madini ujenzi kutokana na wazabuni kutokupeleka vifaa kwa wakati jambo ambalo lina wagharimu katika kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.

Kwa upande wake Scolastika Vitalis ambaye ni mmoja  wa wanakamati wanaosimamia miradi ameileza timu ya menejimenti adha wanayoipata kutokana na wazabuni kutokusambaza madini ujenzi kwa wakati na kuwafanya kukaa uwandani(site) bila kazi yoyote.

Kufuatia changamoto hizo Ndg Magaro ametoa maagizo mazito kwa wazabuni hao ikiwa ni pamoja na kufika kwenye ofisi zao akiwa na timu ya menejimenti na kuwataka kusambaza vifaa kama ambavyo mikataba yao ipo na iwapo watashindwa basi mikataba  yao itaenguliwa na kazi hizo kupewa wazabuni wengine.

Pamoja na hayo Mkurugenzi  amewataka walimu ambao wana simamia miradi hiyo kuhakikisha ubora wa vifaa vinavyoletwa na wazabuni hao  vina ubora unaostahili ikiwa ni pamoja  kusimamia kila hatua ya ujenzi  kwa kushirikiana na kutoa taarifa mahali penye changamoto ili miradi isisimame na wanafunzi waweze kuitumia ifikapo mwakani.

Huu ni utaratibu unaofanywa na Mkurugenzi Mtendaji kwa kushirikiana na timu ya menejimenti kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuendelea kuweka msukumo katika ukamilishwaji wake

Halmashauri ya wilaya ya Geita inaendelea kuishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuleta fedha nyingi kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA VIKUNDI January 23, 2025
  • TANGAZO LA KAZI GEITA DC September 10, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA September 16, 2024
  • Geita Mamlaka za Wilaya na malmaka za miji GP DOM.pdf September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC KOMBA ARIDHISHWA NA UTEKEKEZAJI WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 06, 2025
  • MEI MOSI YALETA FARAJA KWA MAAFISA TARAFA GEITA.

    May 02, 2025
  • RC SHIGELA AIBUA MATUMAINI MAPYA KWA WATUMISHI MKOANI GEITA.

    May 02, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAMPONGEZA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUPATA HATI SAFI

    April 30, 2025
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa