Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Ndg Karia Rajab Magaro Mei 17 ameshiriki Bonanza la Watumishi lililofanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Katoro.
Bonanza hilo lilijumuisha Halmashauri tatu ambazo ni Halmashauri ya Karagwe, Nyang'hwale na Geita ambayo ilikuwa mwenyeji wa michezo hiyo.
Akizindua Bonanza hilo Ndg Magaro amewataka wanamichezo hao kuendelea na maandalizi ya Ushiriki katika SHIMISEMITA.
" Nitoe wito kwa Halmashauri zote Nyang'wale, Karagwe na Geita kuendelea kuwa na maandalizi mazuri kuelekea mashindano ya Michezo ya Watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) ikiwa ni pamoja na kuwa na nidhamu na kuheshimiana.
Vilevile Mkurugenzi Magaro amewaeleza washiriki wa Bonanza hilo kuwa michezo huongeza uwezo wa Kufanya kazi katika maeneo yao wanapotoka.
Bonanza hilo lililokuwa lenye burudani kwa watumishi hao, lilijumuisha michezo ya mpira wa miguu, Pete, kuvuta kamba, kukimbiza kuku na michezo mingine mingi iliyowafanya watumishi hao kufurahi pamoja.
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita
Simu: +225 282520061
Mobile:
Barua pepe: info@geitadc.go.tz
Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa